Sayansi ya Kupata utajiri
5/5
()
About this ebook
Hiki kitabu kitakufundisha sayansi ya jinsi ya kupata utajiri
Sayansi ya kupata utajiri ni kitabu ambacho kimeleta matokeo ya kifedha ya kustaajabisha kwa baadhi ya watu mashuhuri katika dunia ya magharibi. Kinaweza kulinganishwa na vitabu kama The Master Key System cha Charles F. Haanel (1912), Think and Grow Rich cha Napoleon Hill (1937) na vingine vichache. Lakini kipo katika kikundi cha kipekee. Kiukweli , kinajulikana kuhamasisha filamu maarufu ya 2006/2007 ya Rhonda Byrne inayoitwa "The Secret" "Siri". Lakini licha ya hivi vyote, matokeo yake utayagundua katika kufikiri kwako na katika utekelezaji wako kuanzia siku utakayoanza kwenda kwenye undani zaidi wa kurasa zake. Nguvu ya kitabu hiki ipo kwenye matokeo kinayoweza kuyafanya kwenye maisha yako!
Related to Sayansi ya Kupata utajiri
Related ebooks
Mbinu za Kupata Mume Mwema Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsSheria 10 Za Ushawishi Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsItaje! Idai!! Ichukue!!! Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKwa Nini Wakristo Wasiotoa Zaka Huwa Maskini ... Na Jinsi Wanatoa Zaka Wanavyoweza Kuwa Matajiri Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsVile Unavyopaswa Kuwa: kujitambua na kuchukua hatua: Kujitambua, #1 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMafundisho ya Utajiri Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsInamaanisha Nini kuwa na Busara kama Nyoka Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsJinsi Unavyoweza Kutimiza Huduma Yako Rating: 5 out of 5 stars5/5Namna Unavyoweza Kuwa Mkristo Aliyehodari Rating: 3 out of 5 stars3/5Mwenye Kitu Atapewa, Naye Asiye Nacho, Hata Kile Alicho Nacho Tanyang'anywa Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHatua za Ukuaji wa Kiroho Rating: 4 out of 5 stars4/5Ukuaji Wa Kanisa Rating: 5 out of 5 stars5/5Maono Niliyoona Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNdoa ya Mfano Wa Kuigwa Rating: 4 out of 5 stars4/5Laikos: Watenda Kazi wa Kawaida na Huduma Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsSiri za Ushindi Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsEneza Huduma Yako Kwa Miujiza na Udhihirishaji wa Roho Mtakatifu Rating: 4 out of 5 stars4/5Wengine... Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNamna Unavyoweza Kuwa na Muda wa Faragha Mzuri na Mungu Kila Siku Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMpakwa Mafuta na Upako Wake Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWale Wanaosahau Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMti Na Huduma Yako Rating: 3 out of 5 stars3/5Hawara Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWale Wenye Kiburi Rating: 5 out of 5 stars5/5Sanaa ya Kufuata Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMakosa Kumi Makuu Ambayo Wachungaji Wanafanya Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWale ambao ni Wajinga Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsStadi Ya Uongozi Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWaitwao ni Wengi Rating: 4 out of 5 stars4/5Mmoja Wenu Ni Shetani Rating: 0 out of 5 stars0 ratings
Reviews for Sayansi ya Kupata utajiri
1 rating1 review
- Rating: 5 out of 5 stars5/5Kichwa cha habari kimenivutia sana hvyo kama wadau twaweza kushere pamoja
Book preview
Sayansi ya Kupata utajiri - Wallace D Wattles
Iliyochapishwa kwa mara ya kwanza Merekani mnamo 1910 na
Elizabeth Towne Holyoke, Mas. Marekani
Hakimiliki (C) 1910 W.D WATTLE
Hakimiliki (C) Uchapishaji wa AfricanCnturyBooks / Bartahsia 2020
*
Hakimiliki (C) Uchapishaji wa AfricanCnturyBooks / Bartahsia 2020
*
Haki zote zimehifadhiwa. Hakuna sehemu ya toleo hili inayoweza kutolewa nakala kwa njia yoyote au kwa namna yoyote ya elektroniki au mitambo, pamoja na uhifadhi wa habari na mifumo ya kurudisha, bila ruhusa ya maandishi kutoka kwa mchapishaji, isipokuwa na mhakiki ambaye anaweza kunukuu vifungu vifupi kwenye ukaguzi.
Kutoka Kwa Mhariri
Watu wengi wakijua kuhusu maelezo haya ndivyo hivyo maisha ya binadamu yataimarishwa.
* * * * * * *
Mara ya kwanza kusikia juu ya kitabu hiki kidogo nilikuwa naangalia tovuti ya biashara ya mwanamke mmoja anaitwa Tasha. Kusudi langu kwenda kwenye tovuti hii ilikuwa ni kutafuta baadhi ya habari kuhusu mwanamke aliyeibuka kutoka kwenye umaskini na kuwa tajiri.
Sitasahau siku ya kwanza nilipoanza kufyonza maneno ya kitabu hiki. Ilikuwa jioni. Nilikuwa nikisikiliza kwa sauti.
Nakumbuka sikuweza kunyanyuka mahali nilipoketi. Ilikuwa kana kwamba nilikuwa nimeingia katika ukweli mtupu - mahali ambapo uwezekano unajionyesha. Nilipokuwa nikisikiliza, na baadaye nikasoma kitabu hicho, mimi pia nilianza kuuliza swali la Rhonda Byrne - au angalau na mengine tofauti : Inawezaje kuwa sehemu kubwa ya ulimwengu, inaonekana, haina taarifa na kitabu hiki? Inawezaje kwamba hii siri ya wazi sio uasili wa pili kwa kila mwanadamu kwenye sayari - bila kujali lugha, historia ya nyuma au uwezo?
Ni Mungu tu (au ulimwengu ukipenda) ndiye angeweza kuniletea elimu ya kitabu hiki. Na uerevu huo huo,, nina hakika kwamba sasa uerevu huo umeupata.
Kwa maisha yako – kuanzia siku ya leo na kuendelea!
B.A.M TAH
YALIYOMO
1 HAKI YA KUWA TAJIRI
2 KUNA SAYANSI YA KUPATA UTAJIRI
3 FURSA INAWEZA KUTAIFISHWA?
4 KANUNI YA KWANZA KATIKA SAYANSI YA KUPATA UTAJIRI
5 KUONGEZEKA KWA MAISHA
6 NAMNA UTAJIRI UNAVYOKUJIA
7 MOYO WA SHUKRANI
8 KUFIKIRIA KWA NAINA FULANI
9 NAMNA YA KUTUMIA MATAMANIO
10 NAMNA ZAIDI YA KUTUMIA MATAMANIO
11 KUFANYA MAMBO KWA NAMNA FULANI
12 KUFANYA MAMBO KWA UFANISI
13 KUINGIA KWENYE BIASHARA SAHIHI
14 ISHARA YA KUONGEZEKA
15 MTU ANAYESONGA MBELE
16 TAHADHARI NA HITIMISHO LA MAONI
17 MUHTASARI WA SAYANSI YA KUPATA UTAJIRI
UTANGULIZI
Kitabu hiki ni cha uhalisia na sio kifalsafa; Mwongozo wa kitaalam na sio ushauri juu ya nadharia. Imekusudiwa kwa wanaume na wanawake ambao uhitaji wao mkubwa ni pesa; ambao wanataka utajiri kwanza, na falsafa baadaye. Ni kwa wale ambao hadi sasa hawajapata wakati, njia, au fursa ya kwenda kwa undani katika kusoma kwa nadharia, lakini wanataka mafanikio na wako tayari kuchukua matokeo ya sayansi kama msingi wa kazi zao bila kupitia mchakato wowote wa kisayansi.
Inatarajiwa kwamba msomaji atachukua taarifa za kimsingi kwa imani, ni sawa na kuchukua taarifa kuhusu sheria za kanuni za umeme kama zilivyobainishwa na Marconi au Edison; na kwa kuchuchukua taarifa hizo kwa imani, itathibitisha ukweli wao kwa kufanya kazi bila uoga wala kusita. Kila mwanaume au mwanamke anayefanya hivi hakika atakuwa tajiri; kwa maana sayansi inayotumika hapa ni sayansi halisi, na kutofaulu haiwezekani. Hata hivyo kwa faida ya wale ambao wanataka kuchunguza nadharia za falsafa hupata msingi mzuri wa imani, hapa nitataja baadhi ya mamlaka.
Nadharia ya ukweli wa ulimwengu - nadharia ya kwamba moja ni jumla yote na jumla yote ni mmoja, nadharia hii inajidhihirisha vitu vya kilimwengu vinavyo vinavyoonekana ni ya asili ya Kihindu, na kwa taratibu imekuwa ikishinda kwa aina yake mawazo ya nchi zinazoendelea zaidi ya miaka elfu mbili. Ni msingi wa falsafa zote za Mashariki, na zile za Descartes, Spinoza, Leibnitz, Schopenhauer, Hegel, na Emerson.
Msomaji ambaye anaangalia kwa undani misingi ya kifalsafa anashauriwa kusoma Hegel na Emerson; na atafanya vizuri kusoma Habari za Milele,
kijitabu kizuri kabisa kilichochapishwa na JJ Brown, Barabara 300 ya Cathcart, Govanhill, Glasgow, Scotland. Anaweza pia kupata msaada katika safu ya nakala yaliyoandikwa na mwandishi, ambayo yalichapishwa katika Nautilus (Holyoke, Mass.) Wakati wa kiangazi na majira ya joto ya 1909, yakiwa na kichwa cha habari Ukweli ni Nini?
Kwa kuandika kitabu hiki nimecha mambo mengine yote ili niweze kuandika kwa uwazi na lugha rahisi, ili kila mtu aweze kuelewa. Mpango uliowekwa hapa ulitokana na hitimisho la falsafa; imechunguzwa kwa undani, na inaleta matunda mazuri ya majaribio ya vitendo; inafanya kazi. Ikiwa unataka kujua jinsi hitimisho zilifikiwa, soma maandishi ya waandishi yaliyotajwa hapo juu; na ikiwa unataka kuvuna matunda ya falsafa zao kwa mazoea halisi, soma kitabu hiki na ufanye kama vile inavyokuambia ufanye.
Mwandishi.
SURA YA 1
HAKI YA KUWA TAJIRI
Chochote kinachoweza kusemwa kusifu umasikini, ukweli unabaki kuwa haiwezekani kuishi maisha kamilifu au yenye mafanikio kama huna utajiri. Hakuna mwanadamu anayeweza kuinuka kwa kiwango cha juu zaidi katika kipaji au ukuaji wa roho isipokuwa kuwa na pesa nyingi; ili kufunua roho na kukuza talanta lazima awe na vitu vingi vya kutumia, na hawezi kuwa na vitu hivyo isipokuwa tu ana pesa za kununua.
Mwanadamu hukua kiali, kiroho, na kimwili kwa kuwa na matumizi ya vitu, na jamii ina amini kwamba mwanadamu lazima awe na pesa ili aweze kumiliki vitu; kwa hivyo, msingi wa maendeleo yote kwa mwanadamu lazima iwe sayansi ya kupata utajiri.
Lengo kuu la maisha ni maendeleo; na kila kitu kinachoishi kina haki ya kupata maendeleo yote yanayoweza kupatikana.
Haki ya bidamu katika maisha inamaanisha haki yake ya kuwa huru na kutokuzuiliwa matumizi ya kitu chochote ambacho ni muhimu kwakwe kutumia kwama mwanadamu aliekamili kiakili, kiroho na kimwili. Kwa maana nyingine, haki yake ya kuwa Tajiri.
Kwenye kitabu hiki, sitazungumzia juu ya utajiri kwa njia ya mfano; kuwa tajiri sana haimaanishi kuridhika au kutosheka na kidogo. Hakuna mtu atapaswa kuridhika na kidogo ikiwa ana uwezo wa kutumia na kufurahiya zaidi. Kusudi la uasilia ni