Mirathi na Wosia: Utaratibu wa Kufungua, Kusikiliza na Kusimamia Mirathi na Wosia Kisheria Mahakamani: Legal, #1
5/5
()
About this ebook
Elimu kuhusu utaratibu wa kufungua, kusikiliza na kusimamia mirathi na wosia Tanzania ni muhimu. Umuhimu unaongezwa na migongano katika sheria. Sheria zinaratibu aina tatu za mirathi: ya kimila, kiislamu na ya kiserikali. Sheria na taratibu kwa mfano za mirathi ya kimila au ya kiislamu inaweza kukamilisha mirathi mahakamani lakini ikapingwa kwa kutumia sheria nyingine zinazolinda haki za makundi mbalimbali. Mapungufu haya yamechochea umuhimu wa elimu ya utaratibu wa kisheria wa mirathi na wosia kwa makundi mbalimbali Tanzania.
Kitabu hiki kimebainisha sheria zinazohusiana na haki za warithi, taratibu za kupata urithi stahiki, wakfu, haki katika wosia, migongano katika sheria za kimila, kiislamu na za nchi na taratibu za mahakama zinazoweza kurekebisha mapungufu yaliyopo. Kitabu kinatoa mwanga wa namna haki za wahusika mbalimbali katika jamii zinavyolindwa na sheria mbalimbali, taratibu za kudai haki zao, vikwazo wanavyopaswa kuvitarajia, na namna ya kukabiliana na vikwazo hivyo kisheria mahakamani. Kimejengwa kuwa msaada katika kuelezea sheria na taratibu za mirathi na pia katika kubainisha misimamo tofauti ya sheria mbalimbali kuhusu haki za mirathi kwa makundi mbalimbali.
Jumla ya sheria 26, kanuni mbalimbali 11 na kesi 40 zimenukuliwa kuwezesha welewa mpana na kamili. Sehemu ya yaliyomo imebeba mada zote muhimu kumrahisishia msomaji kupata haraka kile anachokitafuta. Mazingira tata na migogoro inayojitokeza mara kwa mara vimeongezwa na kuwasilishwa kwa mpangilio sahili kuwezesha msomaji kupata mwanga wa mambo mbalimbali haraka zaidi.
Kitabu hiki ni msaada mkubwa kwa wanazuoni, wataalamu wa sheria, waheshimiwa mahakimu na majaji katika ngazi zote, na wananchi wa kawaida. Kitabu, pia, kitaongeza mwanga kwa watunga sera na watunga sheria katika maeneo yanayohitaji maboresho kwa ajili ya kujenga mfumo, sheria na taratibu kamilifu na rafiki zaidi za mirathi na wosia Tanzania.
Related to Mirathi na Wosia
Titles in the series (4)
Legal: Legal, #1 Rating: 5 out of 5 stars5/5Lyrical: Legal, #2 Rating: 5 out of 5 stars5/5Love, Luck & Clusterf*ck: Legal, #3 Rating: 5 out of 5 stars5/5
Related ebooks
Afisa Usalama Wa Taifa Ni Mtu Wa Aina Gani? Na Anafanya Nini? Rating: 4 out of 5 stars4/5Kwa Nini Wakristo Wasiotoa Zaka Huwa Maskini ... Na Jinsi Wanatoa Zaka Wanavyoweza Kuwa Matajiri Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNdoa ya Mfano Wa Kuigwa Rating: 4 out of 5 stars4/5Hatua za Ukuaji wa Kiroho Rating: 4 out of 5 stars4/5Namna Unavyoweza Kuwa na Muda wa Faragha Mzuri na Mungu Kila Siku Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHatua Za Kufikia Upako Rating: 5 out of 5 stars5/5Eneza Huduma Yako Kwa Miujiza na Udhihirishaji wa Roho Mtakatifu Rating: 4 out of 5 stars4/5Jinsi Unavyoweza Kutimiza Huduma Yako Rating: 5 out of 5 stars5/5Maono Niliyoona Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKuanzisha Kanisa Rating: 4 out of 5 stars4/5Mpakwa Mafuta na Upako Wake Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNamna ya Kuomba Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHofu Rating: 5 out of 5 stars5/5Itaje! Idai!! Ichukue!!! Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMapepo Na Jinsi Ya Kukabiliana Nayo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsUkuaji Wa Kanisa Rating: 5 out of 5 stars5/5Inamaanisha Nini kuwa na Busara kama Nyoka Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMiaka Miwili Ya Urais Wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Au Nyota Iliyofifia? Rating: 1 out of 5 stars1/5Waitwao ni Wengi Rating: 4 out of 5 stars4/5Jivutie Upako Rating: 4 out of 5 stars4/5Ujasusi Ni Nini? Na Je Majasusi Wanafanya Kazi Gani Hasa? Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsSoma Biblia Yako, Omba Kila Siku ...Ukitaka kukua Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMakosa Kumi Makuu Ambayo Wachungaji Wanafanya Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNyuma Ya Pazia Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNamna Unavyoweza Kuwa Mkristo Aliyehodari Rating: 3 out of 5 stars3/5
Reviews for Mirathi na Wosia
2 ratings1 review
- Rating: 5 out of 5 stars5/5Greatest probate book for Tanzania. The content, high placed reviewers and carefully selected real life questions and answers makes the book excellent in its genre.
Book preview
Mirathi na Wosia - Mgongoro Ernest Jonathan
Mgongoro Ernest Jonathan
GDY PUBLICATIONS COMPANY LTD
S.L.P. 32172
Simu: +255 717326061, 752882235
www.gdypublications.com
info@gdypublications.com
Dar es Salaam
TANZANIA
––––––––
Matini © Mgongoro Ernest Jonathan
Upangaji kurasa © GDY Publications Company Ltd.
Usanifu jalada © GDY Publications Company Ltd.
––––––––
Toleo la Kwanza 2020
––––––––
ISBN 978-9987-452-43-9
––––––––
Haki zote zimehifadhiwa. Hairuhusiwi kuiga, kunakili, kutafsiri au kukitoa kitabu hiki kwa jinsi yoyote ile bila idhini ya GDY Publications Company Limited. Kitabu hiki hakitaazimishwa, kuuzwa kikiwa kimetumika au kukodishwa kibiashara kwa namna yoyote ile zaidi ya makusudi ya uchapwaji wake bila idhini ya GDY Publications Company Limited.
––––––––
Mwandishi: Mgongoro Ernest Jonathan
Mpanga kurasa: GDY Publications Company Ltd.
Aliye sanifu jalada: GDY Publications Company Ltd.
Wahariri: Gabriel D. Kitua, Wigayu Kissandu
Yaliyomo
Shukrani...................................................xii
Virefu vya maneno yaliyofupishwa............................xiv
Sehemu ya kwanza: Mirathi
Utangulizi ..................................................2
Mahakama zinazoshughulikia mashauri ya mirathi...............4
Mahakama za Mwanzo......................................4
Mahakama ya Wilaya (inayokaliwa na Mahakimu Wakazi Wateule wa Wilaya)......5
Mahakama ya Wilaya........................................6
Mahakama Kuu.............................................7
Mali ya ubia..............................................9
Sheria zinazohusu mgawanyo wa mali za marehemu...........10
Msingi wa sheria za mirathi..................................10
Sheria ya Uthibitisho wa Wosia na Usimamizi wa Mirathi....10
Sheria ya Madaraka na Wajibu wa Mtawala Mkuu...........10
Sheria ya Udhamini wa Umma............................11
Sheria ya Watu wenye Asili ya Kiasia wasio Wakristo........12
Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Madai................12
Sheria ya Mirathi ya Kiserikali ya India.....................12
Sheria ya Mtoto.........................................13
Sheria ya Usimamizi wa Haki na Matumizi ya Sheria Mbalimbali ......13
Sheria ya Mahakama za Mahakimu........................13
Sheria zinazohusu mgawanyo wa mali kimila...................13
Kanuni za urithi kimila...................................14
Aina mbili za urithi wa kimila.............................14
Mkondo unaofuata ukoo wa baba ..........................14
Mkondo unaofuata ukoo wa mama..........................16
Watoto waliozaliwa nje ya ndoa...........................17
Sheria ya Mtoto na Haki za Mtoto wa Nje ya Ndoa .............19
Mirathi na watoto wa jinsia ya kike na wajane..............20
Haki ya kurithi ardhi.....................................20
Haki ya mjane mgumba kurithi mali za marehemu mume wake21
Wanapokosekana warithi halali wa marehemu.............22
Sheria zinazohusu mgawanyo wa mali kiislamu..................23
Mgawanyo wa mali kwa njia ya sheria ya Kiislamu ..........24
Daraja la kurithi..........................................25
Wanaostahiki kurithi.....................................26
Viwango vya mgawanyo..................................27
Warithi hawaruhusiwi kurithi kama marehemu anadaiwa ....33
Kuchelewa kugawa mirathi ya kiislamu.....................33
Mali ya wakfu..............................................34
Masharti yanayofanya wakfu uwe sahihi....................35
Msimamizi wa wakfu......................................35
Jinsi ya kuweka wakfu.....................................35
Wanufaika wa wakfu......................................36
Familia.................................................37
Jamii...................................................37
Familia na Jamii..........................................37
Uhusiano na tofauti kati ya wakfu na wosia.................38
Mali ya wakfu Tanzania Bara na Zanzibar...................39
Upande wa Tanzania Bara.................................39
Uandaaji wa wakfu........................................39
Kuanzishwa kwa tume ya wakfu............................40
Maelekezo ya mtoa wakfu lazima yafuatwe....................41
Usajili wa mali iliyo chini ya wakfu...........................43
Nini ufanye mali ya wakfu inapotumika vibaya.................44
Usimamizi wa mali ya wakfu Zanzibar......................45
Utaratibu wa uwekaji wakfu................................45
Masharti ya kukubalika wakfu...............................49
Usajili wa mali za wakfu....................................49
Uendeshaji wa mali za wakfu..............................50
Ukodishwaji wa mali ya wakfu.............................50
Kifo cha mpangaji........................................52
Utaratibu wa kubadili kitu kilichowekwa wakfu.................52
Mambo yanayoathiri uendelezaji wa wakfu....................54
Kufunga wakfu wa familia..................................54
Kumwondoa msimamizi wa wakfu...........................55
Sheria zinazohusu mgawanyo wa mali kiserikali .................55
Sheria ya Urithi ya India...................................55
Sheria ya Uthibitisho wa Wosia na Usimamizi wa Mirathi.....56
Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Madai.................56
Sheria ya Watu Wenye Asili ya Kiasia Wasio Wakristo .......56
Sheria ya Mtoto..........................................56
Mirathi ni haki ya kikatiba.................................57
Sera ya Taifa ya Ardhi ya Mwaka 1995 na Sheria ya Ardhi....58
Mirathi kwa Wakristo.....................................60
Sheria ya mirathi ya Kiislamu na Sheria ya Serikali ..............60
Waislamu wanaohoji sheria ya mirathi ya Kiislamu..........60
Wasiokuwa Waislamu wanaohoji sheria ya mirathi ya Kiislamu61
Utaratibu wa kufungua mashauri ya madai ya mirathi kisheria mahakamani.......63
Taratibu za kufungua maswala ya mirathi Mahakama ya Mwanzo..63
Watu wanaoweza kuwa wasimamizi wa mirathi.............70
Wajibu wa msimamizi wa mirathi.........................71
Utendaji wa msimamizi wa mirathi.........................76
Haki ya msimamizi wa mirathi.............................77
Idadi ya wasimamizi wa mirathi............................78
Wajibu wa mahakama katika kuthibitisha msimamizi wa mirathi.......79
Haki ya warithi dhidi ya msimamizi wa mirathi.............80
Ufafanuzi kuhusu muingiliano kati ya Mahakama ya Mwanzo na ya
Wilaya na Kuu............................................82
Taratibu za kufungua maswala ya mirathi Mahakama ya Wilaya na Mahakama Kuu......83
Utaratibu wa kutoa uthibitisho wa mirathi na hati za usimamizi83
Barua ya maombi ya usimamizi............................85
Utaratibu utumikao katika kuomba barua ya usimamizi .........88
Usimamizi katika mali chache............................91
Uchaguzi wa usimamizi katika mali chache................91
Maombi ya uthibitishwaji wa usimamizi katika mali chache.......92
Uteuzi wa msimamizi wa mirathi katika mali chache ............93
Ukomo wa kufungua mashauri ya mirathi.......................95
Mahakama ya Mwanzo......................................95
Ukomo wa kufungua mirathi katika Mahakamani ya Wilaya na
Mahakama Kuu.............................................97
Ukomo wa madai ya mali isiyohamishika ya marehemu..........97
Uhuru wa kujichagulia sheria ya mirathi ........................98
Pingamizi la taratibu za mirathi..............................100
Mrithi kunyimwa urithi na muusia...........................100
Pingamizi kwa wasii na msimamizi wa mirathi.................101
Mahakama ya Mwanzo..................................101
Mahakama za juu ya Mahakama ya Mwanzo .................102
Utaratibu wa kuweka pingamizi .............................103
Mahakama inaweza kubatilisha au kukataa uteuzi wa msimamizi wa
mirathi .................................................108
Ukomo wa pingamizi (zuio)..................................109
Haki ya mjane kugawiwa nusu ya thamani ya mali aliyoacha marehemu mume wake......111
Utaratibu unaotakiwa kufuata ili mjane apate nusu ya thamani
ya mali ya marehemu mume wake.............................111
Njia za kujenga hoja ya kupata nusu ya thamani ya mali ya
marehemu mume wake ....................................112
Kujenga hoja kutumia sheria ya ndoa......................112
Kutumia sheria za kimila na kanuni za haki za Uingereza....114
Ulinzi wa warithi wanawake kuhusu urithi wao.................116
Hitimisho la sehemu ya kwanza...............................120
Sehemu ya pili: Wosia
Utangulizi..................................................124
Wosia katika sheria mbalimbali...............................126
Wosia katika sheria za kimila................................126
Wosia wa mdomo.......................................126
Wosia wa maandishi.....................................129
Wosia wa Kiislamu..........................................130
Wosia wa mdomo au maandishi............................131
Muusia ana mamlaka ya kutoa zawadi mali yake...........132
Wosia wa kiserikali ........................................134
Wosia wa maandishi.....................................134
Wosia wa mdomo.......................................135
Taratibu za kuandika wosia katika sheria za mirathi.............135
Wosia ..................................................135
Kubadilisha wosia..........................................137
Sehemu salama ya kutunzia wosia............................139
Fomu ya kutunzia wosia ..................................140
Fomu ya kuchukua wosia ................................142
Jinsi ya kutekeleza wosia ..................................143
Uthibitisho wa wosia Mahakama Kuu na Mteule wa Wilaya.......145
Taratibu muhimu za awali ..................................145
Utaratibu wa wosia na barua za usimamizi katika Mahakama Kuu na
Mteule wa Wilaya........................................145
Maombi ya uthibitisho wa wosia Mahakama Kuu na
Mteule wa Wilaya.........................................146
Ombi la kuthibitishwa kwa wosia..........................146
Kuthibitishwa kwa wosia wa mdomo ......................147
Kuthibitishwa kwa nakala ya wosia........................149
Kiapo cha usimamizi wa mirathi..........................149
Kiapo cha mtekelezaji wa wosia .................................... 150
Wosia ulioambatanishwa na barua ya usimamizi wa mirathi..151
Muombaji anapokuwa hajafikisha umri wa mtu mzima.......151
Wosia wa mirathi kwa ajili ya mtu aliyepungukiwa akili......153
Hitimisho la sehemu ya pili...................................155
Sehemu ya tatu: Mifuko ya hifadhi ya jamii
Utangulizi .................................................158
Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi Wa Umma (PSSSF).....160
Aina za malipo..............................................160
Masharti ya malipo..........................................160
Taratibu za kufuatilia malipo..................................161
Maombi ya mafao ya kifo .................................161
Mafao ya Mirathi..........................................164
Pensheni ya urithi.......................................164
Kipindi cha malipo ya pensheni kwa wategemezi...........164
Maombi ya mafao ya mirathi ................................165
Nyaraka zinazotakiwa kuwasilishwa kwa ajili ya kuwezesha mirathi kulipwa......167
Mstaafu aliyefariki akipokea pensheni........................176
Kuchelewa kufungua maombi ya mafao ya mirathi .............177
Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF)......................179
Mafao ya mirathi...........................................180
Pensheni ya urithi ........................................180
Kiwango cha malipo ya pensheni kwa wategemezi..............180
Kipindi cha malipo ya pensheni kwa wategemezi...............180
Sifa zinazotakiwa.........................................181
Aina ya mafao ya pensheni yanayotolewa ..................181
Maombi ya mafao ya mirathi.............................182
Uthibitisho wa mlipwaji akiba (NSSF)......................184
Hitimisho sehemu ya tatu....................................186
Sehemu ya nne: Maswali yanayotatiza na majibu yake
Msimamizi / wasimamizi wa mirathi ..........................188
Uwezo marehemu kuchagua msimamizi......................188
Hivi mume wangu anaweza kuchagua msimamizi wa mirathi yake kabla
hajafa? Msimamizi huyo ni lazima awe kwa maana ya binadamu?......188
Hivi msimamizi wa mirathi ya marehemu lazima awe ndugu wa
marehemu?.............................................189
Tunaweza kuichagua RITA kuwa Msimamizi wa mirathi yetu? .190
Kuteuliwa moja kwa moja na mahakama......................190
Mahakama kuchagua msimamizi.........................190
Mahakama ikimchagua msimamizi wa mirathi ndiyo kazi ya mahakama
imekamilika?.............................................190
Mahakama ikiteua msimamizi wa mirathi, imempa kustahili kurithi mali
yote? ...................................................191
Hivi sheria haisemi kuwa kabla msimamizi wa mirathi hajateuliwa na
Mahakama ya Mwanzo, lazima Mahakama itoe tangazo kwenye magazeti
kuwa anayetaka kupinga uteuzi huo alete pingamzi yake katika miezi mitatu?
Kwa nini wakati mwingine muda wa pingamizi hutolewa mfupi kama wiki
mbili au tatu hivi tu?......................................191
Hivi sheria ya mirathi, inasema msimamizi wa mirathi awe mmoja tu?
Maana nimeona mahakama za mwanzo zinateua msimamizi mmoja tu kila
shauri..................................................193
Je ni sababu zipi zinazoweza kusababisha mahakama ikamuondoa msimamizi
wa mirathi?.............................................193
Sifa za msimamizi wa mirathi ................................194
Sheria imetaja watu wa aina gani ambao wanaweza kuwa wasimamizi wa
mirathi?................................................194
Kuna namna ngapi za utoaji wa mamlaka ya usimamizi wa mirathi?......195
Wosia uliombatanishwa na barua ya usimamizi wa mirathi......196
Kama hakuna wosia .....................................196
Usimamizi wa mirathi kwa mambo maalumu..................197
Utaratibu wa kuomba usimamizi wa mirathi mahakamani........198
Ni Utaratibu gani utumikao katika kuomba usimamizi wa mirathi
mahakamani?...........................................198
Kama kuna wosia wa marehemu ...........................198
Kama hakuna wosia wa marehemu.........................199
Wajibu wa wasimamizi na haki za warithi......................199
Sheria imewapa wajibu upi wasimamizi wa mirathi?........199
Je watu wanaotarajia kufaidika na mirathi wana haki zipi za kisheria
kufuatilia usimamizi wa mirathi?..........................201
Haki ya kumtaka msimamizi asimamie mirathi au ajiondoe.....201
Haki ya kuweka pingamizi.................................202
Haki ya kukagua maendeleo ya kazi ya usimamizi wa mirathi....202
Sheria ipi itumike kwa mirathi ipi? ............................203
Mahakama huamuaje itumie sheria gani kwa mashauri tofauti
ya mirathi.................................................203
Mambo gani huangaliwa kabla ya mahakama kuamua kuchagua kutumia
aina mojawapo ya sheria za mirathi?......................203
Sheria ya mirathi ya kiserikali imetoa utaratibu gani wa kugawa mali?.......203
Urithi wa kimila umegawanywa katika madaraja mangapi? ..204
Daraja la kwanza........................................204
Daraja la pili............................................204
Daraja la tatu...........................................204
Mahakama ipi itumike kwa shauri lipi la mirathi? ...............205
Mashauri yapi ya mirathi yafunguliwe mahakama ipi?...........205
Mahakama zipi zina mamlaka ya kusikiliza masuala ya mirathi205
Mahakama ipi yenye mamlaka ya kufunguliwa mashauri ya mirathi
na katika mazingira yapi?................................206
Mahakama ya Mwanzo ina mamlaka ya kufunguliwa mirathi ya
mabilioni ya fedha? .....................................207
Sheria ya uthibitisho wa wosia na usimamizi wa mirathi inashughulika
na mambo yapi na ina lengo gani hasa?...................208
Haki za wajane na watoto wa kambo..........................209
Kuhusu haki za wajane.....................................209
Kama msimamizi wa mirathi akininyima haki yangu au kupendelea
warithi wengine, nifanye nini?............................209
Mahakama ikiamua kuwa nina haki ya kupata nusu ya mali aliyoacha
marehemu mume wangu, nifanye nini?....................209
Kama marehemu mume wangu alikuwa na kimada na amezaa naye
mtoto au watoto je, naye huyo kimada na watoto wake wanastahili
kurithi sehemu ya mali ya marehemu?....................209
Katika sheria za kimila mjane ana haki ya kurithi?...........211
Haki za watoto wa nje ya ndoa...............................211
Je watoto wa nje ya ndoa wanarithi?........................211
Maswali kuhusu mirathi za kiislamu..........................213
Mirathi panapokuwa na mke aliyepewa talaka na wategemezi wengine.......213
Pale wasii anapogawa mali kwa upendeleo na wengine kutopata marehemu anapoacha mke na watoto......213
Pale marehemu anapoacha hisa ya mali, mama, watoto 3 wa kike
na wa kiume na ndugu...................................213
Watoto wa mke wa kwanza wanapoona mirathi baada ya miaka 12, ili
hali marehemu aliwaandikia nyumba watoto wa mke wake wa mwisho......214
Pale mama anapoacha mali akiwa na watoto wanne, lakini kabla ya umauti aliolewa na mme mwingine ambaye hakubahatika kupata mtoto........214
Kama marehemu aliacha watoto wa kiume na wakike wa wake zake wawili wa ndoa na mke mkubwa alimuacha marehemu kabla ya umauti, je
watoto wake wanayo haki?...............................215
Ikitokea mume ameamua kuoa bila cheti cha ndoa kinachotambulika
kisheria, akafariki, je mke (mjane) anaweza kuwa mrithi halali?215
Ikiwa baba na mama wanaweza kurithiana, na mtoto anaweza
kumwandikia mama yake mali kabla ya kufa kwake kama zawadi?.......216
Je, inafaa kurithi wazazi wasio Waislamu?..................216
Je Uislamu unakubali mgao wa mali nyingine na theluthi ya mali kumpa mtoto wa kurithi (adopted)?.......217
Sehemu ya tano: Fomu mbalimbali za kisheria kuhusu mirathi na wosia
Fomu zinazotumika katika utaratibu wa kuendesha mashauri ya mirathi katika Mahakama Kuu, Wilaya Na Mahakama Ya Mwanzo.......219
Mahakama ya Mwanzo.....................................219
Chini ya Sheria ya Mahakama za Mahakimu 1963 Nyongeza ya 5, 1984........219
Fomu zinazotumika katika uthibitisho wa wosia na
usimamizi wa mirathi (barua ya usimamizi katika
Mahakama Kuu, Wilaya, Mahakama ya Wilaya
na Mahakama ya Hakimu Mkazi.)..............................220
Sheria ya uthibitisho wa wosia na usimamizi wa mirathi katika
kanuni ya uendeshaji mirathi, Jedwali la kwanza chini ya kifungu
cha 9 cha sheria ya Uthibitisho wa Wosia na Usimamizi wa Mirathi
sura ya 352 ya toleo la 2002...............................220
Fomu za wosia na wakfu.....................................268
Sheria ya usajili wa Nyaraka Sura ya 117 toleo la 2002..........268
Fomu zinazotumika katika usimamizi wa mali ya
wakfu na amana Zanzibar...................................268
Fomu za mifuko mbalimbali ya hifadhi ya jamii.................269
Mfuko wa Penshion kwa Watumishi wa Umma (PSSSF).........269
Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF)......................276
Mashauri yaliyo nukuliwa....................................278
Sheria na kanuni zilizo nukuliwa...............................281
Faharasa..................................................284
Marejeo ya ziada...........................................286
Kutabaruku
Kwa mke wangu mpendwa Getrude Vedastus Mahendeka na watoto wangu wapendwa Jovin Ernest Mgongoro na Ivynna Ernest Mgongoro
Shukrani
Kwanza kabisa, namshukuru Mwenyezi Mungu Kwa kuniwezesha na kunifungua akili nikaandika kitabu hiki.
Pia namshukuru Mh. Dickson Augustino Mmasi Hakimu Mkazi, Mh. Shija Mdadila Hakimu Mkazi, Mh. Nicosemu Mwakibibi Hakimu Mkazi, Mh. George Kazi Jaji wa Mahakama Kuu ya Zanzibar, Mh. Jaji John Samwel Mgetta Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania kwa michango na mawazo yao ya kuboresha kitabu hiki.
Vile vile namshukuru Baba Askofu wa Jimbo la Tunduru – Masasi, marehemu Mhashamu Baba Askofu Castor Paul Msemwa kwa kunipa nafasi kutoa mada inayohusu Sheria ya Mirathi na haki za mjane kurithi nusu ya mali waliyochuma pamoja na mume wake, katika kongamano la Umoja wa Wanawake Katoliki Kanda ya Kusini. Namshukuru Sheikh wa mkoa wa Rukwa, Sheikh Rashid Akilimali kwa kunipa muongozo wa Sheria za Mirathi kwa upande wa sheria ya kiislam. Pale palipopunguka Imam Athuman Hemid Fumo, Imam wa Masjd Annas Mtonga, Korogwe alipajazia vyema. Nicodemus. N. N. Nditi (Jr) mkufunzi wa Taasisi ya Mafunzo ya Kisheria kwa Vitendo (LST) na Msemo Mavale – wakili na mkufunzi wa muda wa Taasisi ya Mafunzo ya Kisheria kwa Vitendo (LST) kwa michango yao mizuri katika rasimu ya mwisho.
Uongozi wa NSSF na wa PSSSF kwa pamoja wametoa mchango mkubwa katika kukamilisha sehemu ya tatu ya kitabu - mifuko ya jamii.
Kwa namna ya pekee sana, ningependa kuwashukuru Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria na Kabidhi Wasii Mkuu. Mamlaka hizi mbili zilipitia kwa kina rasimu ya kitabu hiki na kuwasilisha mapendekezo yao ya maboresho.
Wizara ya Katiba na Sheria walikuwa wa kwanza kukamilisha upitiaji wa rasimu. Katika barua yao ya tarehe 21 May 2020, kumbukumbu namba AB.75/297/01/22, Wizara ilimpongeza mwandishi kwa kazi nzuri ikisema kitabu kitakuwa msaada mkubwa na kwa watu wengi. Barua pia ilisema kuwa kitabu kinagusa maisha ya kila siku ya mwananchi wa kawaida. Zaidi ya pongezi, Wizara ilitoa mapendekezo ya maboresho ambayo yote yalizingatiwa kwa umakini katika kukamilisha kitabu hiki. Baada ya maboresho na uwasilishaji wa maelezo ya jinsi mapendekezo ya maboresho yalivyoingizwa, Wizara ilitoa pongezi tena kwa mwandishi na mchapishaji kwa kazi nzuri. Pongezi hizi za pili ziliwasilishwa kupitia barua ya tarehe 24 Agosti 2020 iliyokuwa na kumbukumbu namba AB.75/297/01/48.
Katika barua ya kumbukumbu namba BC.206/272/01/55 ya tarehe 28 Juni 2020, ofisi ya Kabidhi Wasii Mkuu ilitoa maoni kuwa kitabu kitakuwa msaada kwa jamii kwa sababu kinaelezea maswala ambayo ni chanzo cha migogoro katika jamii za Tanzania. Ofisi ya Kabidhi Wasii Mkuu pia iliwasilisha mapendekezo ya maboresho ambayo yote yazingatiwa kwa umakini wakati wa kukamilisha toleo hili la kitabu.
Timu nzima ya jopo la uhariri likiongozwa na Bw. Gabriel D. Kitua, Afisa Mtendaji Mkuu wa GDY Publications Ltd. pamoja na Bi. Wigayu Kissandu, mwanasheria kutoka Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake (WLAC) walifanya kazi kubwa katika kuhakikisha kuwa kitabu kinakamilika kilivyostahili. Ni kwa kupitia mapitio kadhaa na utekelezwaji wa maboresho mengi ndipo tukaweza kuwa na kitabu unachokifurahia sasa mkononi mwako.
Mwisho lakini sio kwa umuhimu, nawashukuru Rose Silvester Matofali na Astrida kwa kuchapa kurasa nyingi za kitabu hiki.
Virefu vya Maneno Yaliyofupishwa
AC – Appeal Cases
BK – Baada ya Kristo
EA – East Africa
EALR – East African Law Report
FN – Namba ya Fomu
FLR – Federation Law Report (US)
GN – Government Notice
HCD – High Court Digest (Tanzania)
H.J. – Hijiria
L&R – Law and Report.
LRT – Law Reports of Tanzania.
LAPF – Local Authorities Pension Fund (Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Serikali za Mitaa)
Mh. – Mheshimiwa
Na. – Namba
n.k. – na kadhalika
NPF – National Provident Fund
NSSF – National Social Security Fund (Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii)
PSSSF – Public Service Social Security Fund (Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma)
RITA – Registration Insolvency and Trusteeship Agency (Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini)
Shs – Shilingi.
T – Tanzania
TLS – Tanzania Law School
TRL – Tanzania Law Report
Uk. – ukurasa
U.S – United State of America
WLAC – Women’s Legal Aid Centr
Sehemu ya Kwanza
Mirathi
Utangulizi
Tanzania ni nchi inayotambua uwepo wa taratibu tofauti za kufungua mirathi kwa kuzingatia maisha ya watu, mila, desturi na dini wanazoabudu. Uzoefu umeonesha kuwepo kwa matatizo mengi katika familia au ukoo pale mtu anapofariki, matatizo hayo hutokana na maswali ya msingi ambayo yatajibiwa katika sura hii. Maswali hayo ni kama yafuatayo:
a) Warithi halali wa mali za marehemu ni akina nani?
b) Nani mwenye haki ya kusimamia mirathi ya marehemu?
c) Je mjane/mgane aliyeachwa ana haki ya kurithi au kupata chochote katika mirathi hiyo?
d) Ni sheria zipi zitatumika katika masuala ya mirathi?
e) Nini wajibu wa msimamizi wa mirathi katika kusimamia mali za marehemu?
f) Wajibu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii katika kushughulikia mirathi ya mwananchama wake ni upi?
Pamoja na kuwepo na sheria za kimila, sheria ya Kiislamu na sheria ya Kiserikali, nchi yoyote pia husimamiwa na kuongozwa na katiba. Mirathi ni haki ya kikatiba kama ilivyoainishwa katika ibara mbalimbali ndani ya katiba na hakuna mtu, taasisi au serikali yenye mamlaka ya kuzipora haki hizo. Ibara ya 13 (1), (2)[1] inatamka kuwa:
13(1) Watu wote ni sawa mbele ya sheria, na wanayo haki, bila ya ubaguzi wowote, kulindwa na kupata haki sawa mbele ya sheria.
(2) Ni marufuku kwa sheria yoyote iliyotungwa na mamlaka yoyote katika Jamhuri ya Muungano kuweka sharti lolote ambalo ni la ubaguzi ama wa dhahiri au kwa taathira yake.
Mirathi maana yake ni kuondoa umiliki kutoka kwa mtu aliyekufa kwenda kwa warithi walio hai, kama kilichoachwa ni mali au haki miongoni mwa haki za kisheria[2] Mirathi ni mali inayohamishika (mfano: fedha na gari) na isiyohamishika (mfano: nyumba na shamba) vinavyoachwa na marehemu ambavyo hupewa warithi wake kwa kufuata taratibu zilizopo kisheria. Aidha, mirathi inajumuisha mafao ya mtumishi aliyefariki ambayo hulipwa kwa familia yake au ndugu zake marehemu kwa kuzingatia Sheria ya Mirathi. Sura hii itajadili sheria ya mirathi zinazotumika Tanzania bara, utaratibu wa kufungua mirathi, kusikiliza na kusimamia mirathi kisheria mahakamani.
Sura hii itajadili sheria za mirathi zinazotumika Tanzania bara na pia itagusia baadhi ya sheria za mirathi zinazotumika Tanzania visiwani haswa upande wa mali za wakfu zinazosimamiwa na Sheria ya Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana namba 2 ya 2007 inayohusu Zanzibar pekee. Lengo ni kuonesha jinsi gani sheria hizi zinafanya kazi kwa ukaribu haswa upande wa mali za wakfu zinazowalenga Waislamu.
Sura ya 1: Mahakama Zinazoshughulikia Mashauri ya Mirathi
1.1. Mahakama za Mwanzo
Mahakama ya Mwanzo inayo mamlaka katika masuala yote yanayohusu usimamizi wa mirathi inayotokana na wosia na ile isiyotokana na wosia yenye asili ya sheria ya kimila na kiislam[3].
Sheria za mirathi zinazotumika katika Mahakama za Mwanzo ni sheria za Kimila na Kiislam pamoja na kanuni mbalimbali za uendeshaji mirathi.
Kanuni za utaratibu wa kufungua mashauri ya mirathi katika Mahakama za Mwanzo zilizotungwa chini ya Sheria ya Mahakama za Mahakimu[4], ndio zinazotumika katika kuendesha mashauri ya mirathi. Pia Mahakama za Mwanzo ni lazima zifuate utaratibu uliooneshwa katika Tangazo la Serikali Na. 49 la 1971. Mashauri ya Fanuel M. Ng’unda dhidi ya Herman M. Ngund’a na wengine[5], Richard J. Rukambura dhidi ya Isack N. Mwakajila na wengine[6] na Shomvi Uliza dhidi Mwajabu Rajabu[7] yanaainisha kanuni ifuatayo:
Mahakama ya Mwanzo inayo mamlaka katika masuala yote yanayohusu usimamizi wa mirathi yenye asili ya sheria ya kimila na Kiislamu. Hii ni kwa mujibu wa kifungu cha 19 cha sheria ya Mahakama ya Mahikimu na utaratibu wa kusikiliza mashauri ya mirathi umeainishwa katika jedwali la 5 la sheria ya Mahakama ya Mahikimu.
Mahakama ya Mwanzo inayo mamlaka ya kusikiliza shauri la usimamizi wa mali chache endapo mali ya mtu wa kabila fulani zitasimamiwa kutokana na sheria za kabila hilo isipokuwa kama marehemu katika muda wowote alikuwa ni mfuasi wa dini ya kiislam[8]. Vifungu vya sheria hii ya uthibitisho wa wosia na usimamizi wa mirathi[9] havitumiki katika usimamizi wa mali ambazo Mahakama ya Mwanzo haina mamlaka isipokuwa kama mwenendo kuhusiana na urithi wa usimamizi wa mali chache umeanza katika Mahakama ya Mwanzo, Mahakama Kuu inaweza kutoa maelekezo kuwa iendelee kusikilizwa katika Mahakama ya Mwanzo au kuhamisha kwa kutumia kifungu cha 47[10]
Ikiwa agizo la kusimamia mali limefanywa na, au mwenendo kuhusiana na mirathi umeanzishwa katika Mahakama ya Mwanzo, Mahakama Kuu haitatoa agizo lolote, isipokuwa kama ikiona ni sawa katika maslahi ya haki au kwa ulinzi wa mnufaishwaji yeyote au mdai mali hiyo isimamiwe kwa kutumia sheria hii[11].
1.2. Mahakama ya Wilaya (inayokaliwa na Mahakimu Wakazi Wateule wa Wilaya)
Jaji Mkuu anaweza kuteua Mahakimu Wakazi wa Mahakama ya Wilaya kusikiliza mashauri ya mirathi kama Mahakimu Wateule[12]. Mahakimu Wateule watakuwa na mamlaka katika mashauri yote yanayohusu mirathi na usimamizi wa mirathi huku wakiwa na mamlaka ya kuteua msimamizi wa mirathi na kutoa hati ya usimamizi wa mirathi ikiwa kama marehemu katika kipindi cha kifo chake alikuwa akiishi katika eneo ambalo hakimu huyo aliteuliwa. Pia watakuwa na mamlaka kurekebisha au kutengua mirathi hiyo[13]. Kama ilivyoamuliwa kwenye shauri la Shomari Abdallah dhidi ya Abdallah HusseinnaHassani Ramadhani[14],
"Shauri hili kwanza lilifunguliwa katika Mahakama ya Mwanzo lakini baada ya kugundulika kuwa Mahakama haina mamlaka, kumbukumbu zilitumwa Mahakama ya Wilaya ikasikilizwa na Hakimu Mkazi. Mrufani hakuridhika na maamuzi ya Hakimu Mkazi hivyo alikata rufaa Mahakama Kuu. Mahakama Kuu iliamua kuwa:
Ili Hakimu Mkazi aweze kusikiliza mashauri ya Wosia inabidi akae kama Hakimu Mkazi Mteule wa Wilaya aliyeteuliwa na Mh. Jaji Mkuu kwa mujibu wa kifungu cha 5 cha Sheria ya Uthibitisho wa Wosia na Usimamizi wa Mirathi Sura ya 352 Chapisho la 2002.
Pasipo kifungu cha 5 cha sheria hii, sura ya 352, iwapo Hakimu Mkazi atasikiliza shauri la Wosia na Mirathi kwa mujibu wa sheria hii sura ya 352 chapisho la 2002 na hajateuliwa maamuzi yake yatakuwa batili."
Mahakama ya Wilaya inayokaliwa na Hakimu Mkazi Mteule wa Wilaya inayo mamlaka ya kusikiliza mashauri ya mirathi yasiyozidi thamani ya Sh shilingi elfu kumi na tano (15,000/=), zaidi ya thamani hiyo basi Mahakama ya Wilaya inayokaliwa na Hakimu Mkazi Mteule wa Wilaya italazimika kutoa taarifa Mahakama Kuu ya Tanzania ili itoe maelekezo mengine aidha kutoa kibali kwa mahakama ya Wilaya inayokaliwa na Hakimu Mkazi Mteule wa Wilaya kuendelea kusikiliza shauri hilo[15].
1.3. Mahakama ya Wilaya
Mahakama ya wilaya, itakuwa na mamlaka katika usimamizi wa mirathi ya mali chache, pale ambapo marehemu amefia katika sehemu ambayo Mahakama ina mamlaka[16]. Mahakama ya Wilaya ina mamlaka ya kusikiliza mashauri ya usimamizi wa mali chache zenye thamani isiyozidi shilingi za kitanzania milioni mia moja (Tshs. 100,000,000/=)[17]. Katika shauri la Ashura M. Masoud dhidi ya Salma Ahmad[18], Mahakama Kuu iliamua kuwa,
"Mamlaka ya Mahakama ya wilaya katika suala la mirathi na usimamizi imeelezwa