Mwongozi Wa Roho: Safari Maishani
By Ken Luball
()
About this ebook
Mwongozi wa Roho
Related to Mwongozi Wa Roho
Related ebooks
Anagkazo (Nguvu ya kushurutisha!) Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMwana-Adam ni Nani Naye ni Nini Mungu Amkomboe: Chuo cha Kwanza, #1 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsRoho Mtakatifu Rating: 5 out of 5 stars5/5Wakristo:Mabalozi wa Ufalme wa Mungu Maagizo Kuhusu Kuishi kama Mkristo. Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsSauti Ya Mungu Yenye Nguvu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWengine... Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsVitengo vya Ujenzi Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsStadi ya Usikivu [toleo la 2] Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHistoria & Maisha ya Yeshua Kristo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKusamehe Kumerahisishwa Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHatari za Kiroho Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWale ambao ni Wajinga Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMaono Niliyoona Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWaambie Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNguzo za Imani Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsLaikos: Watenda Kazi wa Kawaida na Huduma Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsSiri ya Dhabihu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWale wanaokushitaki Rating: 5 out of 5 stars5/5Wale Wanaojifanyisha Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsYisrael Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMrembo, Mnyama na Mchungaji Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsBadilisha Huduma yako ya kiuchungaji Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsBinti Unaweza Kufanikiwa Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsJinsi ya Kusali & Kuongea na Yahweh Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsImani Kwa Wale Walioitwa na Kuchaguliwa na Mungu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMmoja Wenu Ni Shetani Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMguso Mzuri Wa Upako Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMambo ya Kufanya Saa Yako Ikifika Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsUkweli Muhimu Kwa Ajili Ya Waumini Wapya Rating: 3 out of 5 stars3/5Inamaanisha Nini kuwa na Busara kama Nyoka Rating: 0 out of 5 stars0 ratings
Reviews for Mwongozi Wa Roho
0 ratings0 reviews
Book preview
Mwongozi Wa Roho - Ken Luball
Mwongozi wa Roho: Safari Maishani
––––––––
Riwaya ya Kiroho na Ken Luball
& Bodhi ( Mwongozi wa Kiroho
)
––––––––
Translator: Samwel Lubisia
Copyright Claimant: Ken Luball
Ujumbe wa mwandishi:
Nini Maana ya Uzima?
Maana ya uzima,
Sababu tupo hai,
Ni kumusikiliza kimya kimya kwa makini Roho aliye ndani yetu ,
Na kuifuata katika njia atakayotuongoza.
Vipo vitabu vinne katika Tetralojia ya Kuamka
:
Leo Naenda Kufa: Uchaguzi Maishani
Mwongozi wa Roho: Safari Maishani
Utulivu: Kijiji Cha Matumaini
Mauzauza ya Raha: Kuchagua Upendo badala ya Hofu
Maisha ya kiroho ni hali ya ni kuamini yuko Mungu (Roho au Nafsi) katika kila maisha, na kwa sababu hii maisha ya kila mmoja ni muhimu , ni sawa na yameunganishwa.
Lengo langu la kukiandika kitabu hiki ni Kuwaamsha na kuwasaidia wengine Walioamka, kuelewa kikamilifu maana ya Kuona Nuru, na kwa hivyo, Safari yao katika Maisha inaweza kutambulika kikamilifu.
Hadithi tatu zimeandikwa katika nafsi ya kwanza, kufuatilia safari ya Kiroho
Maishani mwa mtoto. Wanapopata mafunzo ya jinsi ya kuyajibu maswali hayo [niliyouliza mwanzo] kwa njia ya kueleweka, kuvutia, na ya kipekee, ambayo sio tu ya kufikirisha bali pia kusisimua.
Bodhi ni Mwongozi wangu wa Kiroho
; ananizungumzia kwa urahisi huku nikiandika mawazo yake. Japo safari yangu ya Kuiona Nuru, haijakamilika, Bodhi, akiwa Mwongozi wa Roho, Bila Shaka Amelimika. Tulikiandika kitabu hiki kwa ajili ya wote wanaotaka kuianza safari ya Kuamka au Wameamka na wanatafuta njia ya Kuiona Nuru
Ni kwa upendo tu na msaada wa Bodhi
tuliweza kuviandika vitabu hivi kwa pamoja
Japo Mwongozi Wa Roho ni hadithi ya kubuni, ningependa ufikirie hili, kwa kuwa Bodhi alikuwa mhusika mkuu kwangu pamoja na Amara katika kitabu hiki, Mwongozi wa Roho. Yamkini hadithi inayosimuliwa huenda isiwe ya kubuni, ila iliyo halisi. Kwa kuwa hadithi hii nilisimuliwa
na Bodhi, alivyokuwa Mwongozi wa Roho hapo awali kwa Amara, nadhani uwezekano wa kila kitu anachosema, na onyo anazojaribu kuwasilisha, ni halisi na kweli, hadithi hii inaweza kuwa kweli pia.
Ili kujua mengi kuhusu vitabu vyote vinne katika Tetralojia hii katika wavuti wangu http://kenluball.com .
Dibaji:
Hatua Tatu za Kuona Nuru
Hatua ya kwanza – Usingizi (Kulala)
Hatua ya kwanza huanza tunapozaliwa,
Tunapojumuishwa
na Kufunzwa
tunayofaa
Kuamini
(Ego) tunavyoendelea kuyaona na Kukubali
mengi kutoka kwa jamii tulivyozaliwa kwayo.
Tunapozaliwa, picha iliyopo hapo juu inaonyesha kwamba
Utambulisho wetu tayari hua umeamuliwa.
Rangi ya ngozi yetu, nchi tunayozaliwa, Dini na ulinganisho mwingine wowote ulioundwa na binadamu
Huamua mustakabali wetu ulimwenguni.
Tunaamini
ulinganisho huu ni wa kweli kwa kuwatazama wengine,
Kusoma kuwahusu kwenye vitabu na magazeti na kuwatazama katika Runinga na Filamu.
Watu wengi hukubali tofauti hizi na kuzifanya sehemu yao,
Au wanaenda zaidi kudhibitisha
Kwamba wao ni bora na wa maana zaidi kuliko wengine.
Wanaoyakubali na kuyaamini wanayofunzwa
Kuwa ya kweli, hubakia wamelala
licha ya mafaniko
yao Maishani, hatima yao ni maisha duni ya kiwango cha chini sana.
Wanaamini furaha na maana itatoka ulimwenguni,
Kamwe haiwezi [kutoka ulimwenguni].
Hatua Ya Pili –Kuamka
Wanaoamka huanza kudadisi kila Tulichojifunza
na Kukubali
kuwa halisi na kweli maishani Tulipokuwa tukikua wakubwa.
Wale ambao Huamka
huanza kudadisi ikiwa kila kitu Tulijifunza
Na Kukubali
kuwa halisi maishani, tulipokuwa tukikua, ilikuwa kweli.
Hisia inaanza kukua ndani yetu, Haiwezi kupuuzwa tena,
Kuhoji uhalisia wa Kila kitu tulichoamini hapo awali.
Ingawa tunaweza kuwa tunaishi maisha yenye Mafanikio
, tuna utajiri, tuna umaarufu, Au ulinganisho mwingine wowote wa Kujifunza kuhusu Mafanikio ni nini, Haiondoi tena hisia za wasiwasi tulonazo
Zinatoka Ndani
yetu.
Uchungu tunaohisi unatoka kwa Roho wetu, aliye maishani mwa kila kitu.
Wengine wanaweza kumwita Roho Mungu/Nafsi hai au kumpa jina lingine; haijalishi.
Inawakilisha Mwongozi
wetu maishani na huyapa maisha yetu Maana
.
Tunaamka
pindi tu tunapohisi kuna jambo lisilo sawa,
Tunaanza kudadisi kama yote tulojifunza na kukubali kuwa kweli huenda hayakuwa kweli,
Basi hatuna budi kuianza safari yetu,
Safari ya Kuona Nuru.
Hatua Ya Tatu – Kuona Nuru.
Tunaelimika pindi Tunapokubali
Kwamba kila
jambo tulojifunza na Kuamini kuwa kweli hakika haikuwa kweli.
Licha ya jinsi Tunavyoonekana, Mali yetu, Kazi, Vitu tunavyomiliki
Au mengine yote tuliyofunzwa yanatofautisha na wengine, tunang'amua sasa kwamba hatuko bora au wa maana zaidi kumliko yeyote.
Tunaanza Kuiskia
Roho aliye ndani mwetu, Tunaukumbatia ujumbe wake kwa kushiriki Upendo Wetu bila Masharti na wote.
Japo tuliyojifunza (Ego) tukiwa wadogo daima inasalia nasi,
Ushawishi wake hubaki finyu.
Badala ya kushindana, sasa tunashirikiana.
Badala ya kuishi kwa hofu, tunaazimia kuishi kwa upendo.
Badala ya kutamani yaliyo bora kwa ajili yetu tu,
Sasa tunatamani kuwasaidia wengine bila ubinafsi,
Kurahisisha safari yao
maishani.
Kwa madiliko na Kukubali
ujumbe wa Roho tunaendelea kuifuata njia yetu ya Kuona Nuru.
Table of Contents
Sura Ya 1: Kusudi Langu Maishani
Sura Ya 2: Roho
Azaliwa
Sura Ya 3: Nafsi
Yazaliwa
Sura Ya 4: Nafsi Nzuri
Sura Ya 5:Uhusiano wa Roho na Nafsi
Sura Ya 6: Kutawaliwa na Nafsi.
Sura Ya 7:Miaka Mitano Ya Kwanza Maishani
Sura Ya 8:Kuishi Maisha Chanya
Sura Ya 9:Kuishi Katika Ulimwengu wa Mwanga
Sura Ya 10: Mafanikio Maishani ni Nini?
Sura Ya 11: Vijimambo vidogovidogo Visikutoe Roho
Chapter 12: Happiness and Love
Sura Ya 13:Maisha Ulimwenguni kote
Sura Ya 14:Mafunzo Maishani
Hitimisho: Safari ya mwandishi (Ken) maishani
Kumhusu Ken
Sura Ya 1:
Kusudi Langu Maishani
N
itakutambia hadithi tofauti na yoyote ambayo umewahi kusikia hapo awali. Hadithi hii itasimuliwa na "Mwongozi wa Roho", ambaye, katika Safari hii Maishani, yupo ndani ya msichana mdogo anayeitwa Amara, jina ambalo lina maana ya milele
katika lugha ya kale ya Sanskrit ya India. Hadithi hii itafuata maisha yake, tangu wakati yeye ni kijuzi tu ndani ya mamake, hadi kifo chake miaka mingi baadaye. Hadithi yenyewe nitakusimulia mimi, ambaye ni Mwongozi wake wa Roho; jina langu ni "Bodhi".
Nina uhakika una hamu ya kujua zaidi kidogo kunihusu, hivyo kabla nianze hadithi yangu, nitajieleza kidogo. Jina langu ni "Bodhi, ambalo katika lugha ya Sanskrit humaanisha
Kuamka au
Kuona Nuru." Nimekuwa Mwongozi wa Roho kwa muda wote wa maisha; Viongozi wa Roho ni wa milele. Kusudi Langu Maishani ni kusaidia kiumbe hai katika Safari yake Maishani, kwa kushiriki maarifa yangu nao. Kwanza najiunga na maisha kabla hawajazaliwa nabaki ndani yao, katika Safari yao Maishani, hadi wanapoiaga dunia. Ninaponza, niko hapa kumsaidia Amara. Kusudi langu ni kushiriki naye maarifa ya maisha, ili aweze kupata Maana, Kuelewa na Upendo usio wa Masharti maishani mwake. Mwongozi wa Roho ni nguvu na msukumo uliopo katikati ya maisha; kwa Amara, kama ilivyo kwa wengine wengi, nitakuwepo ndani ya Moyo wake. Ndani ya nguvu yangu, yapo maarifa mengi ya historia ya ulimwengu. Hekima yote, ya milele, ipo ndani yangu, kama ilivyo ndani ya kila Mwongozi wa Roho. Sababu yangu kuwepo, katika Safari hii Maishani, ni kumsaidia Amara kuelewa kusudi la maisha yake. Niko hapa ili ajifunze kutoka kwangu na ashiriki haya na wengine; kwa kushiriki Kiini changu na Upendo wangu na wengine bila ubinafsi, maisha yake yatakuwa yamekamilika. Atazaliwa na maarifa yote atakayohitaji kuishi maisha ya furaha, yenye maana; atazaliwa "Amelimika". Hii ndiyo sababu kila Mwongozi wa Roho yupo, na Safari yetu Maishani itafanikiwa tu ikiwa tunaweza kutimiza hili ili tuweze kuyapa maana maisha ambayo tupo kusaidia.
Amara atakiandika kitabu hiki muda mfupi kabla ya kuaga dunia, miaka mingi baada ya kuzaliwa. Hadi wakati huo, mara nyingi alishindwa kusikia mawazo yangu vizuri. Kila mmoja ana Mwongozi wake wa Roho, hivyo unaweza kufikiria jinsi tulivyo wengi. Kwa kuwa Mwongozi wa Roho hajawahi kuandika kitabu kamwe, nadhani ni muhimu kukujulisha kwanini nachukua hatua hii isiyo ya kawaida. Ninaelewa jinsi ilivyo vigumu kuamini ninachokuambia; hata hivyo, singewahi kamwe kujitambulisha na kukiandika kitabu hiki, kwa msaada wa Amara, kama haingebidi kabisa.
Niko hapa kukuonya. Mabadiliko yasipokuja haraka, maisha yote katika sayari hii yanaelekea kikomo. Pupa, inayowakilishwa na tamaa iliyokithiri kwa wengi ili wapate utajiri, imesababisha vita, chuki, hofu, njaa, ukosefu wa makazi, dhana sisizo za uhakika, mabadiliko ya Tabianchi, vifo visivyo na maana na mengine mengi; haya yote yanatishia maisha. Vitisho vingi vinavyoweza kuleta mwisho wa haraka wa maisha ni sababu moja tu ya kitabu hiki kinaandikwa. Pia kinaandikwa kukujulisha jinsi janga hili linaweza kuepukika. Dunia iko kwenye ukingo wa hali ya hatari sana. Ingawa muda unakimbia na kuisha vilivyo, hatujachelewa sana kubadilisha athari inayotukodolea macho. Ili kufanya hivyo, hata hivyo, ni