Mambo ya Kufanya Saa Yako Ikifika
()
About this ebook
Saa yako kufika haimaanishi saa katika damu na nyama, kama vile saa saba mchana au saa ya kula chakula bali inamaanisha saa katika ulimwengu wa roho. Saa ni kipimo cha muda, katika ulimwengu wa mwili na ulimwengu wa roho pia, lakini katika ulimwengu wa roho saa inasomwa kutokana na matukio. Kwa mfano, watu wanaweza kusema huyu amepona ajali mbaya kwa sababu saa yake haijafika.
Na ninaposema mambo ya kufanya saa yako ikifika siyo lazima iwe saa ya kufa kwako lakini saa au siku ya kufikwa na jambo fulani ambalo limekuwa likisubiriwa katika ulimwengu wa roho. Saa yako ikifika katika ulimwengu wa roho huwa ni kama mtihani pia. Ukivuka kwa ufaulu unaenda kiwango kingine cha juu zaidi na ngazi njema zaidi katika Kristo Yesu. Katika kitabu hiki utajifunza mambo ya kufanya ili uweze kufaulu mtihani wako saa yako ikifika.
Msafiri J. Mwaikusa
MSAFIRI J. MWAIKUSA is an assistant pastor at a local Assemblies of God church in Dar es Salaam, Tanzania, where he lives with his wife, Tracy, and their children. He also hosts a weekly podcast named Biblia Inasema Usiogope which can be listened to through Radio Public, Google Podcast, Apple Podcast and other platforms. He holds a bachelor degree in Bible and Theology from the Global University of Springfield MO, U.S.A; Msafiri has an MBA and business experience in food industry and publication. He also has a teaching experience from the University of Dar es Salaam where he obtained his Bachelor of Science in Molecular Biology and Biotechnology.
Read more from Msafiri J. Mwaikusa
Biblia Inasema Usiogope Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMbinu za Kupata Mume Mwema Rating: 0 out of 5 stars0 ratings
Related to Mambo ya Kufanya Saa Yako Ikifika
Related ebooks
Kushindwa Sasa Basi Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMwanzo: Kitabu cha Mianzo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWakristo:Mabalozi wa Ufalme wa Mungu Maagizo Kuhusu Kuishi kama Mkristo. Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsSauti Ya Mungu Yenye Nguvu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsJinsi ya Kusali & Kuongea na Yahweh Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNguzo za Imani Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsAnagkazo (Nguvu ya kushurutisha!) Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMwana-Adam ni Nani Naye ni Nini Mungu Amkomboe: Chuo cha Kwanza, #1 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsRoho Mtakatifu Rating: 5 out of 5 stars5/5Mwongozi Wa Roho: Safari Maishani Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsSiri ya Dhabihu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKatika Eneo la Adui Kuokolewa na Silaha ya Siri: Swahili Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsImani Kwa Wale Walioitwa na Kuchaguliwa na Mungu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsYisrael Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHistoria & Maisha ya Yeshua Kristo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKondoo Aliye Potea Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsUpendo wa Mungu na Msamaha Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWengine... Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsVitengo vya Ujenzi Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKitabu cha Sherehe Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWale Wanaojifanyisha Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsGUNDUA UCHUKUZI WAKO Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKurudi Nyuma Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKitabu Cha Mistari Ya Bibilia Ya Kukari Rating: 3 out of 5 stars3/5Laikos: Watenda Kazi wa Kawaida na Huduma Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMguso Mzuri Wa Upako Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWale Wana ambao ni Hatari Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsBinti Unaweza Kufanikiwa Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsStadi ya Uchungaji Rating: 2 out of 5 stars2/5Kuanzisha Kanisa Rating: 4 out of 5 stars4/5
Related categories
Reviews for Mambo ya Kufanya Saa Yako Ikifika
0 ratings0 reviews
Book preview
Mambo ya Kufanya Saa Yako Ikifika - Msafiri J. Mwaikusa
DIBAJI
Mara nyingi katika maisha huwa kuna mambo yanatokea ambapo inakuwa ni kama saa yako imefika. Hii saa yako kufika haimaanishi saa katika damu na nyama, kama vile saa saba mchana au saa ya kula chakula bali inamaanisha saa katika ulimwengu wa roho. Saa ni kipimo cha muda, katika ulimwengu wa mwili na ulimwengu wa roho pia, lakini katika ulimwengu wa roho tunaweza kusema saa pia tukimaanisha siku. kwa mfano watu wanaweza kusema huyu amepona ajali mbaya kwa sababu siku
yake haijafika lakini maana hiyo hiyo inaweza kufikishwa kwa kusema saa
yake haijafika.
Kwa hiyo ninaposema mambo ya kufanya saa yako ikifika siyo lazima iwe saa ya kufa kwako lakini saa au siku ya kufikiwa na jambo fulani ambalo limekuwa likisubiriwa katika ulimwengu wa roho. Pengine huweza kuitwa saa ya kujiliwa au siku ya kujiliwa au hata majira yako. Naongelea jambo ambalo linaweza kuwa kama mwisho au hitimisho wa mtiririko wa matukio fulani ambayo yamekuwa kama yakikuandaa kufika hapo mahali au saa hiyo. Kwa mfano, katika ulimwengu wa mwili mwanafunzi aliyeanza darasa la kwanza mpaka darasa la saba unaweza kusema siku yake ni ile siku ya mtihani wa mwisho kabisa wa darasa la saba. Yaani kama vile kuhangaika kote kwa miaka saba ya kusoma sasa kunafika tamati kwa tukio la kufanyika mitihani ya darasa la saba. Nadhani hapo utaweza kuelewa vizuri nini ambacho nalenga katika somo hili.
Majira haya au siku au saa yako ikifika katika ulimwengu wa roho huwa ni kama mtihani pia. Ukivuka kwa ufaulu unaenda kiwango kingine cha juu zaidi na ngazi njema zaidi kwa kadiri kiongozi wetu Kristo Yesu anavyoona inafaa kwa utukufu wa Mungu Baba.
Sasa basi tuangalie mambo ya kufanya saa yako ikifika.
UTANGULIZI
Kitabu hiki cha Mambo ya Kufanya Saa Yako Ikifika kimetokana na somo la Kibiblia. Ingawa tutakuwa tunaangalia mistari mbalimbali katika Biblia, msingi hasa wa somo lenyewe umetoka kwenye Kitabu cha Injili kama ilivyoandikwa na Yohana sura ya 12 mstari wa 20-30
20 Palikuwa na Wayunani kadha wa kadha miongoni mwa watu waliokwea kwenda kuabudu kwenye sikukuu.
21 Basi hao walimwendea Filipo, mtu wa Bethsaida ya Galilaya, wakamwomba, wakisema, Bwana, sisi tunataka kumwona Yesu.
22 Filipo akenda, akamwambia Andrea; kisha Andrea na Filipo wakamwambia Yesu.
23 Naye Yesu akawajibu, akasema, Saa imefika atukuzwe Mwana wa Adamu.
24 Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi.
25 Yeye aipendaye nafsi yake ataiangamiza; naye aichukiaye nafsi yake katika ulimwengu huu ataisalimisha hata uzima wa milele.
26 Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu.
27 Sasa roho yangu imefadhaika; nami nisemeje? Baba, uniokoe katika saa hii? Lakini ni kwa ajili ya hayo nilivyoifikia saa hii.
28 Baba, ulitukuze Jina Lako. Basi ikaja sauti kutoka mbinguni, Nimelitukuza, nami nitalitukuza tena.
29 Basi mkutano uliosimama karibu wakasikia, walisema ya kwamba kumekuwa ngurumo; wengine walisema, Malaika amesema naye.
30 Yesu akajibu, akasema, Sauti hiyo haikuwako kwa ajili yangu, bali kwa ajili yenu.
(Yohana 12:20-30)
Kwa hiyo mara kwa mara tutakuwa tunarejea kwenye kipande hiki cha Injili na kutoa jambo muhimu la kuangalia. Mambo ya kujifunza kutoka kwenye sehemu hiyo ya Injili ni mengi lakini kwa sasa ni haya tu ambayo Roho wa