Imani Kwa Wale Walioitwa na Kuchaguliwa na Mungu
()
About this ebook
Mada ya imani ni muhimu sana kwetu kuelewa. Kitabu hiki kinashughulikia misingi ya kile tunahitaji kuelewa juu ya imani. Soma kitabu hiki ili ujue jinsi ya kuongeza imani yako. Maandiko mengi yaliyonukuliwa yanatuonyesha kile Biblia inafundisha juu ya imani, na maoni kwa wakati wote ambayo yanamwongoza msomaji kuelewa maandiko ambayo yamenukuliwa.
Kitabu hiki kinafundisha juu ya mfano wa Mababa wetu wa Imani, kama vile Ibrahimu. Matendo yao yanaonyesha kuwa walikuwa na imani iliyo hai na tunaona wanapongezwa kwa hili. Imani yetu lazima iwe ya matendo na hai pia. Tunajifunza kuwa imani sio tamaa - hisia za kawaida lakini jambo lenye nguvu na hatua. Unaweza kushangazwa na baadhi yay ale yanayofundihshwa na Biblia katika suala la kuwa na imani. Kitabu hiki kifupi kitakuonyesha maandiko haya na kukusaidia kuelewa maana ya kuwa mwaminifu.
Kitabu hiki kinatusaidia kugundua jinsi wafuasi wa Kristo wanapaswa kukuza imani, ambayo ni kwa mujibu wa imani katika Neno – yaani Biblia. Tunajifunza mambo kadhaa ya kushangaza juu ya imani, yaliyothibitishwa kupitia Maandiko. Je! Ulijua kuwa msamaha kwa wengine unahusiana na imani? Kitabu hiki kinashughulikia maoni potofu ya kawaida juu ya imani na Sheria na inaelezea wazi ukweli wa jambo hili kwa kutumia Maandiko na mfano wa matendo. Utasoma ahadi na maagizo ya Mungu wa Milele aliye hai, kama ilivyoandikwa katika Biblia, ambayo inaweza kujenga imani yako. Utajifunza kuwa mambo yanayodhaniwa kuwa hayawezekani, mambo ambayo hatujawahi kufikiria, tunapokuza imani yetu, yanawezekana - kwa sababu tu tuna Baba mwaminifu ambaye ni Mungu wa kuamini. Imani hii yetu inaweza kutuathiri hapa na sasa na vile vile nyakati ambazo ziko mbele.
Watu ambao watakuwa na Mfalme wa Wafalme wakati atakaporudi wanaitwa, kuchaguliwa na ni waaminifu. Ikiwa unataka kuwa mmoja wa wachache ambao hupatikana kuwa waaminifu wakati wa mwisho ni muhimu kujenga uhusiano wako na Muumba wa Ulimwengu, kitabu hiki kinaweza kukusaidia. Soma kitabu hiki na utafute maandiko yaliyoonyeshwa. Kitabu hiki kinaweza kutumika kama rejeleo na kusomwa tena na kurudiwa ili kuelewa imani na kuiweka imani hiyo kwa matendo.
Bob Thiel, Ph.D.
Dr. Thiel has a Ph.D. in one of the sciences and a foreign Th.D. in early Christianity. As the overseeing pastor of the Continuing Church of God, he works with people around the world to work on Jesus' commissions in Matthew 24:14 and Matthew 28:19-20, as well as working on other matters written about in the New Testament.
Related to Imani Kwa Wale Walioitwa na Kuchaguliwa na Mungu
Related ebooks
Katika Eneo la Adui Kuokolewa na Silaha ya Siri: Swahili Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKurudi Nyuma Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsVitengo vya Ujenzi Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWengine... Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWale Wanaojifanyisha Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWale ambao ni Wajinga Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMguso Mzuri Wa Upako Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNi Jambo Zuri Sana Kumtumikia Bwana Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKusamehe Kumerahisishwa Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWakristo:Mabalozi wa Ufalme wa Mungu Maagizo Kuhusu Kuishi kama Mkristo. Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsSiri ya Dhabihu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsJinsi ya Kusali & Kuongea na Yahweh Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsRoho Mtakatifu Rating: 5 out of 5 stars5/5Kondoo Aliye Potea Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMwongozi Wa Roho: Safari Maishani Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWale Wana ambao ni Hatari Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsYisrael Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsBinti Unaweza Kufanikiwa Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHistoria & Maisha ya Yeshua Kristo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsLaikos: Watenda Kazi wa Kawaida na Huduma Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsStadi ya Uchungaji Rating: 5 out of 5 stars5/5Mmoja Wenu Ni Shetani Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMrembo, Mnyama na Mchungaji Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWale wanaokushitaki Rating: 5 out of 5 stars5/5Waambie Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsGUNDUA UCHUKUZI WAKO Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNguzo za Imani Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsStadi ya Usikivu [toleo la 2] Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNamna Unavyoweza Kuwa Mkristo Aliyehodari Rating: 3 out of 5 stars3/5Mpakwa Mafuta na Upako Wake Rating: 0 out of 5 stars0 ratings
Reviews for Imani Kwa Wale Walioitwa na Kuchaguliwa na Mungu
0 ratings0 reviews
Book preview
Imani Kwa Wale Walioitwa na Kuchaguliwa na Mungu - Bob Thiel, Ph.D.
Imani Kwa Wale
Walioitwa na
Kuchaguliwa na Mungu
Na Bob Thiel,SU.
Copyright 2014 by Nazarene Books.Toleo la kwanza.Kijitabu kinachotolewa na Kanisa la Mungu Linaloendelea (CCOG) na warithi wake,shirika la mtu binafsi.1248 E.Grand Avenue#,Arroyo Grande,Carlifornia,93420 USA.
Maandiko yamenukuriwa kutoka kwa New King James Version (Thomas Nelson,Copyright 1997;yanatumika kwa idhini) wakati mwingine hufupishwa kama NKJV,lakini kwa kawaida huonyeshwa bila ufupisho.
ISBN 978-1-940482-04-0
Jalada:Miguu juu ya maji inaonyesha kwamba Wakristo wanapaswa kutembea kwa imani si kwa kuona (2 Wakorintho 5:7).Jalada la nyuma inaonyesha Bahari ya Galilaya.Mtume Petro aliitwa na kuchaguliwa na hata alitembea na Yesu kwa muda mfupi juu ya maji (Mathayo 14:25-31).Licha ya kutembea juu ya maji,Petro alikuwa na imani ndogo,na Yesu alimhimiza awe na imani zaidi.
Imani Kwa Wale
Walioitwa na
Kuchaguliwa na Mungu
Na Bob Thiel,SU.
Imani ni nini? Je! Imani inaweza kuongezwa?
Je imani ni hisia tu?Je! Imani inabatilisha amri?
Wengi wanaongea juu ya imani,lakini je!Ni kweli wana imani?
Mamilioni wamekosa imani ya kuyapokea majibu ya maombi.
Mara nyingi ni kwa sababu ya kukosa kuelewa maana ya imani.
Je! Waweza kusoma na kufanya yaliyofundishwa na Biblia kuhusu imani?
Imani kwa wale walioitwa na kuchaguliwa na Mungu
Je! Wajua zaidi kuhusu imani? Je! Wajua jinsi imani ni ya muhimu?
Yesu alisema,ya kwamba pamoja na rehema na hukumu,imani ni moja ya masuala yenye uzito na ya maana sana ya amri (Mathayo 23:23).Wanafunzi wake waligundua kwamba imani ni muhimu.
Siku moja:
5…Mitume wakamwambia Bwana,’’Tuongezee imani’’ (Luka 17:5,NKJV isipokuwa mahali pameonyeshwa sehemu:hata hivyo kijitabu cha Imani ni nini? Kimenukuriwa kutoka kwa KJV,bila ilani iliyotengwa.)
Bila kuwaambia jinsi ya kuongeza imani yao,Yesu aliwaambia kwamba walikuwa na imani duni.
Lakini katika sehemu nyingine za Biblia,Yesu na wengine walieleza kwa kina jinsi imani inaweza kuongezwa.Hiki kijitabu kifupi kitaeleza vipengele vingi lakini si vyote.Biblia ya Kiingereza ya NJKV,kwa mfano,ina neno la Kiingereza ‘’imani’’ mara 243 katika Agano Jipya (mara mbili katika Agano la Kale) na neno uaminifu