Discover millions of ebooks, audiobooks, and so much more with a free trial

Only $11.99/month after trial. Cancel anytime.

Tishio la Ukombozi: Ubeberu na Mapinduzi Zanzibar
Tishio la Ukombozi: Ubeberu na Mapinduzi Zanzibar
Tishio la Ukombozi: Ubeberu na Mapinduzi Zanzibar
Ebook297 pages3 hours

Tishio la Ukombozi: Ubeberu na Mapinduzi Zanzibar

Rating: 0 out of 5 stars

()

Read preview

About this ebook

Tishio la Ukombozi examines the role of the Umma Party of Zanzibar and its leader in the turbulent years of the Zanzibar revolution of the 1960s that was perceived in those Cold War years as a threat to the interests of the US and Europe. Based on declassified US and British documents, in-depth interviews and information released by WikiLeaks, A

LanguageKiswahili
PublisherDaraja Press
Release dateSep 22, 2016
ISBN9780995222335
Tishio la Ukombozi: Ubeberu na Mapinduzi Zanzibar
Author

Amrit Wilson

Amrit Wilson was Senior Lecturer in Women's Studies/South Asian Studies at Luton University. She set up the first Asian women's refuge in London and works with 'Asian Women Unite'. She is author of Finding A Voice (Virago, 1978), which won the Martin Luther King award, and has written about black experiences in Britain, the politics of South Asia and gender issues. She is the author of Dreams, Questions, Struggles (Pluto, 2006) and The Threat of Liberation (Pluto, 2013).

Related to Tishio la Ukombozi

Related ebooks

Reviews for Tishio la Ukombozi

Rating: 0 out of 5 stars
0 ratings

0 ratings0 reviews

What did you think?

Tap to rate

Review must be at least 10 words

    Book preview

    Tishio la Ukombozi - Amrit Wilson

    Tishio la Ukombozi

    Tishio la Ukombozi

    Ubeberu na Mapinduzi Zanzibar

    Amrit Wilson

    Tafsiri ya Kiswahili: Ahmada Shafi Adam

    Daraja Press

    Montreal

    Kimechapishwa na Daraja Press

    www.daraja.net

    © Hakimiliki 2016 Amrit Wilson

    ISBN: 978-0-9952223-2-8

    Haki zote zimehifadhiwa, isipokuwa pale ilipoainishwa vyenginevyo. Hakuna sehemu yoyote ya kitabu hiki inayoweza kunakiliwa au kusambazwa kwa njia yoyote ile, ikiwa kwa mitambo au barua-pepe pamoja na fotokopi au kwa mfumo wowote wa kurekodi, kuhifadhi au kutumia maelezo, bila idhini ya maandishi ya wachapishaji.

    Mfasiri: Ahmada Shafi Adam

    Mchoraji-jalada: Kate McDonnell

    Picha: Babu aliyotolewa kutoka gerezani Aprili 29, 1963 © Corbis

    1

    Kwa Kumkumbuka Babu

    Na Kwa Watu Wa Zanzibar Ambao Mapambano Yao Bado Yanaendela

    Contents

    Orodha ya Picha

    Shukrani

    Vifupisho

    Utangulizi

    1. Siku za Awali za Mapambano Dhidi ya Ukoloni

    2. Waingereza Wakabidhi Madaraka kwa Sultani na Washirika Wake

    3. Mapinduzi ya Zanzibar na Hofu za Wabeberu

    4. Muungano na Tanganyika

    5. Utawala wa Kidikteta wa Karume

    6. Kesi Katika Mahakama Bandia ya Zanzibar

    7. Zanzibar na Bara Katika Kipindi cha Mfumo Huru Mambo Leo

    8. Uingiliaji Kati wa Marekani Zanzibar na Bara Hivi Sasa

    Nyongeza Ya Kwanza

    Nyongeza Ya Pili

    Rejea

    2

    Orodha ya Picha

    Babu mara baada ya kurejea kutoka London mwaka 1957, 28

    Wanafunzi wa kike wanachama wa YOU waliopigwa picha na Waingereza waliokuwa na wasiwasi na ‘vijana wakakamavu’, 30

    Accra, Mkutano wa Nchi zote za Afrika 1958, 38

    Babu akiwasili katika sherehe za kusherehekea kuachiwa kwake kutoka gerezani tarehe 29 April, 1963, 51

    Kundi kubwa la watu likisubiri kwa hamu kumkaribisha Babu mbele ya makao makuu ya Chama cha ZNP, Darajani mkabala na jengo la Bharmal, 52

    Babu akiwa na Karume, 62

    Che Guevara na Babu, wakipumzika baada ya Mkutano wa Kwanza wa Maendeleo ya Kibiashara wa Umoja wa Mataifa (UNCTAD), Geneva, Julai 1964, 65

    Malcolm X na Babu katika Hadhara ya Mkutano wa Umoja wa Wamarekani wenye Asili ya Afrika, New York, Disemba 13 1964

    Tarehe 10 Februari 1965, Babu wakati huo akiwa waziri wa biashara na Lin Hai-yun, kaimu waziri wa biashara za nje wa China walitia saini mkataba wa biashara na itifaki kuhusu ubadilishanaji wa bidhaa mali  kwa mali kati ya China na Tanzania. Hapa tunawaona wakibadilishana nyaraka walizozisaini wakati huo, 84

    Babu na Makamo wa Rais Kawawa wakiwa na mashujaa wa matembezi marefu, Januari 1965, 85

    Ndani ya Ukumbi Mkuu wa Umma, Beijing, 1965. Mstari wa mbele kutoka kushoto: Mashal Chen Yi, Babu, Rais Liu Shaoqui, Makamo wa Rais wa Tanzania Kawawa, Mwenyekiti Mao Zedong, Silo Swai (Tanzania), Waziri Mkuu Zhou Enlai, George Kahama (Tanzania), 86

    Babu akijaribu kuelezea mtazamo wake wa kiuchumi kwa Nyerere, 87

    Kuachiwa kwa Makomred wa Chama cha Umma bara. Waliosimama mstari wa mbele, kutoka kushoto kwenda kulia: Babu, Martin Ennals kutoka Shirika la Kimataifa la Kutetea Haki za Binadamu (Amnesty International), Ali Mahfoudh, Hashil Seif Hashil; mstari wa pili, kutoka kushoto kwenda kulia, Suleiman Mohamed (Sisi), Salim Saleh, Haji Othman, Shaaban Salim, Tahir Ali; mstari wa tatu, kutoka kushoto kwenda kulia Amour Dugheish, Martin Hill kutoka Shirika la Kimataifa la Kutetea Haki za Binadamu (Amnesty International), Abdulla Juma, Badru Said, Hamed Hilal; nyuma ya mstari wa tatu ni Ahmed Mohamed (Tony), 115

    Babu na Tajudeen Abduraheem, katibu mkuu wa Mkutano Mkuu wa Saba wa Umajumui wa Afrika na vijana wengine wanaharakati wa Vuguvugu la Umajumui wa Afrika, mwezi Machi 1994, 116

    Badawi Qullattein, Hashil Seif Hashil na Khamis Ameir Zanzibar, Juni 28, 2012, 160

    3

    Shukrani

    Ingawa ni mimi niliekiandika Kitabu hiki lakini kwa sehemu kubwa sana kinatokana na juhudi za pamoja zilizozaliwa kutokana na fikra na tafkari za pamoja kupitia kwa Makomredi wenzangu, Khamis Ameir, Shaaban Salim na Hamed Hilal, ambao wote walikuwa ni makada wa Chama cha Umma Party. Sio tu walitowa maelezo juu ya harakati zao zilizopita lakini pia walichangia katika kukusanya nyaraka na picha pamoja na kutoa ufafanuzi wa matukio mbalimbali. Kwa hivyo ni kitabu chetu kwa pamoja, ni chao kama kilivyokuwa ni changu. Juu ya hivyo ni mimi peke yangu ninaechukuwa jukumu la makosa yoyote yatakayoweza kujitokeza katika kitabu hiki.

    Ningelipenda pia kuchukuwa fursa hii kumkumbuka na kumuenzi Komredi wetu mpenzi Marehemu Qullatein Badawi, aliyetushajiisha na kutusaidia katika juhudi zetu za kukitafiti kitabu hiki. Ninamshukuru Hashil Seif Hashil ambae pia alikuwa ni kada wa Chama cha Umma Party kwa kunipa maelezo kuhusu harakati zake za kisiasa.

    Katika kipindi nilichokuwa nikiandika kitabu hiki, Narendra Gajjar ndiye mtu aliekuwa nikiwasiliana nae sana. Kila mara akihakikisha kuwa tayari kunijibu maswali yangu kwa njia ya simu au barua-pepe, na bila ya kusita kunipatia mawasiliano na watu mbali mbali, nyaraka za kuvutia na fikra juu ya njia za kufanya kuweza kupata majibu ya masuala magumu na/au yaliyokuwa na utata.

    Miongoni mwa wengine wengi walionisaidia ningelipenda kutowa shukurani zangu kwa Mohamed Saleh na Salma Maoulidii kwa kunipatia maandishi na machapisho yao, Mailys Chauvin kwa kunisaidia katika kuhakiki maelezo mbali mbali wakati alipokuwa Zanzibar pamoja na kuniruhusu kutumia picha yake ya Khamis, Badawi na Hashil iliyochukuliwa katika mwaka 2012. Ninamshukuru pia Firoze Manji kwa kunipa moyo katika kipindi ambacho sikuwa na uhakika kama mswaada wangu ungeliweza siku moja kuchapishwa na kuwa kitabu.

    Shukrani zangu pia kwa wachapishaji wa Pluto Press na hususan Anne Beech kwa msaada wake na usahihishaji wake makini na wa kina.

    Kwa tafsiri hii ya Kiswahili, shukrani zangu za kipekee za dhati ya moyo wangu ziwaendee Ahmada Shafi Adam aliyefanya kazi nzuri ya kukitafsiri kitabu, na Mohamed Saleh aliekihariri, pamoja na Mansab Abubakar, Firoze Manji, na Ludovick Mwijage waliowezesha uchapishaji wake.

    Hatimae, ningelipenda kuishukuru aila yangu kwa kusoma na kudadisi sura mbali mbali za mswaada zinazofuata – bila ya shauku yao na kunipa moyo kwao kitabu hiki kamwe kisingeliweza kukamilika.

    Amrit Wilson

    4

    Vifupisho

    Vifupisho

    AAPC All African People’s Conference

    AFRICOM United States Africa Command

    AGA AngloGold Ashanti

    AIMP Association for Islamic Mobilisation and Propagation

    ANC African National Congress

    AOPIG African Oil Policy Initiative Group

    ASP Afro-Shirazi Party

    ASU Afro-Shirazi Union

    ATA Anti-Terrorism Assistance

    CCM Chama cha Mapinduzi

    CIA (US) Central Intelligence Agency

    CMOs Civil Military Operations

    CT Counterterrorism

    CUF Civic United Front

    DCM Deputy Chief of Mission

    DfID Department for International Development (UK)

    DRC Democratic Republic of Congo

    EAC East African Community

    EALA East African Legislative Assembly

    EPZ Export Processing Zone

    FDI Foreign Direct Investment

    FPTU Federation of Progressive Trade Unions

    FRTU Federation of Revolutionary Trade Unions

    GOT Government of Tanzania

    ICFTU International Confederation of Free Trade Unions

    IMF International Monetary Fund

    MIGA Multilateral Investment Guarantee Agency

    MOU Memorandum of Understanding

    MPLA People’s Movement for the Liberation of Angola

    NASA National Aeronautics and Space Adminstration (US)

    NGO Non-Government Organisation

    NPT Non-Proliferation Treaty

    OAU Organisation of African Unity

    PAC Pan Africanist Congress

    PAFMECA Pan African Freedom Movement for East and Central Africa

    PLA People’s Liberation Army

    PNUSS Party for National Unity for the Sultan’s Subjects

    REDET Research and Education for Democracy in Tanzania

    SEZs Special Economic Zones

    SWAPO South West Africa People’s Organisation

    TANU Tanganyika African National Union

    TAZARA Tanzania-Zambia Railway

    tcf trillion cubic feet

    TIC Tanzanian Investment Centre

    TPDC Tanzania Petroleum Development Corporation

    TPDF Tanzanian People’s Defence Force

    UNCTAD United Nations Conference on Trade and Development

    UNDP United Nations Development Programme

    URTZ United Republic of Tanganyika and Zanzibar

    YOU Youths Own Union

    ZAPU Zimbabwe African People’s Union

    ZNP Zanzibar Nationalist Party

    ZPFL Zanzibar and Pemba Federation of Labour

    ZPFTU Zanzibar and Pemba Federation of Trade Unions

    ZPPP Zanzibar and Pemba People’s Party

    5

    Utangulizi

    Ni mahali pa ‘vituko vilivyoandaliwa vyema’, na safari za kuchunguza mazingira, ‘ni pepo ambayo jina lake tu huleta dhana ya kula njama; hivi ndivyo Zanzibar inavyoelezwa siku hizi. Kwa kiasi kikubwa, katika kipindi cha mwongo uliopita wa miaka ya 2000, Visiwani, kama visiwa viwili vya Zanzibar (Unguja na Pemba) vinavyoitwa, vimeuzwa ili kuwa kiwanja cha michezo kwa watalii kutoka nchi za magharibi. Hapa ndipo mahali ambapo tunatakiwa tuamini, kuwa panaanza na kumalizika kwa yale tuyaonayo leo, bila ya kuwa na yaliyopita ambayo yalikuwa na umuhimu wowote wa kisiasa au mustakabali wenye tofauti yoyote na yale ya hivi sasa. Hata historia yake inapatikana kama vidonge vya dawa vilivyofungashwa vizuri kwa matumizi ya watalii.

    Lakini kama zilivyo ‘pepo’ nyingi za aina hiyo, kwa watu wanaoishi humo ukweli uko tofauti kabisa. Kwao, mambo kadha ya zamani ambayo bado yamo katika kumbukumbu zao yanaendelea kujitokeza tena hivi sasa.  Ndani ya chombo kinachowasafirisha watu baharini kutoka Dar es salaam kwenda Unguja na kurudi, kikundi cha vijana wanabishana kwa jazba juu ya mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964 na yaliyotokea baada ya hapo, juu ya athari za muungano wa Zanzibar na Tanganyika uliofuatiwa na kuundwa kwa Tanzania, na michango ya Julius Nyerere, Abdulrahman Mohamed Babu na Abeid Karume. Katika magazeti yanayotolewa kila siku, matukio ya miaka ya 1960 na 1970 yanaendelea kuzusha mijadala mikali. Machungu ya wale waliowapoteza watu wao wanaowapenda na hasa njia za kuendeshea maisha yao katika kipindi kilichoshuhudia mabadiliiko hayo na matokeo ya kusikitisha yaliyofuatia mapinduzi hayo yanajitokeza katika maoni mbalimbali, majadiliano, kumbukumbu na mitandao ya kijamii. Na mikahawani, wale wasiopendelea chama chochote, ikiwa Chama cha Mapinduzi (CCM) au Chama cha Wananchi (CUF) hufanya utani juu ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa iliyoanzishwa kwa shinikizo kutoka nchi za magharibi ambayo hivi sasa ina umri wa miaka minne na tayari imeanza kufanya nyufa. Watu hao husema kuwa, maafa yanarudiwa yakiwa mithili ya kichekesho. Wakati huo huo, kila mtu anaelewa juu ya kuwepo kwa jeshi la Marekani nchini. Wanafungua skuli, wanatoa tunzo na kujiimarisha visiwani, kwasababu, kama zilivyofichua nyaraka za siri zilizotolewa na Wikileaks ambazo zinaeleza kuwa, sasa, kama ilivyokuwa wakati wa mapinduzi ya 1964 na vita baridi, Zanzibar, kwa mara nyengine tena inaonekana kuwa ni kipande muhimu cha mchezo wa dama unaochezwa na Marekani kupitia sera zake za nchi za nje na za kijeshi katika Bara la Afrika.

    Uingiliaji wa Marekani katika mambo ya ndani ya Zanzibar baada ya mapinduzi una vitu vingi vinavyofanana na uingiliaji wa hivi karibuni kabisa wa Marekani katika Bara la Afrika. Kusema kweli, mambo mengi ya mtindo uliobuniwa wakati wa vita baridi bado yanaendelea kutumika hadi hivi leo. Kama ilivyokuwa wakati wa machafuko ya Libya, nchini Zanzibar vile vile Marekani ilifanya kila juhudi ili ionekane kama kwamba ni ‘matakwa ya Afrika’. Lakini wakati NATO iliingilia kati na kuivamia Libya kupigana na majeshi ya Gaddafi, Visiwani Zanzibar Marekani iliisukuma Uingereza kuingilia kati na kuandaa Mpango wa Utekelezaji wa Zanzibar ambao ungeliwawezesha kuwashawishi kwa kuwatumilia akili wale viongozi inaoweza kuwachezea ili waiombe Uingereza iingilie kati kijeshi.

    Kwa nini uingiliaji kati huo haukutokea wakati wa, au mara tu baada ya machafuko ya Zanzibar? Kwa kiwango fulani, ilikuwa ni kwasababu ya kuwepo kwa chama cha kimapinduzi kilichoandaliwa vizuri kabisa, chama cha Umma Party. Ijapokuwa chama hiki sicho kilichoyaanzisha mapinduzi ya Zanzibar, chama cha Umma Party kiliyageuza mapinduzi ya Zanzibar kutoka kuwa maasi ya kihuni na kuwa upinzani wa kimapinduzi, na kuchukua madaraka ya dola na kuyadhibiti mnamo saa chache. Ama kuhusu umbile la mapinduzi yenyewe, kwa kila hali yalikuwa ni ya kwanza ya aina yake katika Afrika ya leo. Wakati nchi za Afrika, isipokuwa Kenya na Algeria, zilipata uhuru kwa njia ya majadiliano (visiwani Zanzibar, Waingereza walimkabisdhi madaraka Sultani) mapinduzi ya Zanzibar yalikuwa ndiyo ya kwanza kuupindua utawala wa serikali ya ukoloni mambo leo. Hapa, kama alivyoandika kiongozi wa Chama cha Umma Party, Abdulrahman Mohamed Babu, watu walikuja juu siyo kwasababu ya kuipindua serikali iliyofilisika kisiasa na mfalme wa kikaragosi tu bali pia walifanya mapinduzi ili kuubadilisha mfumo wa kijamii ambao uliwakandamiza na kwa mara ya kwanza kuchukua majaaliwa ya historia yao katika mikono yao wenyewe (Babu, 1989: 3).

    Kurasa zinazofuata zinaelezea njia iliyofuatwa na chama cha Umma Party na makada wake, kwa kutumia ushahidi wa picha za kihistoria, mahojiano, na zile zilizokuwa nyaraka za siri za Marekani na Uingereza. Tunachunguza juu ya namna gani chama kiliibuka kutoka katika wimbi la maandalizi ya kupambana na ukoloni ili kukabiliana na watawala waliokabidhiwa madaraka na Uingereza wakati wa uhuru, na namna gani kilipanga mikakati ya kujenga umoja katika Zanzibar iliyokuwa imegawika kikabila (Angalia Sura ya 1 kwa mjadala juu ya ukabila na matabaka Zanzibar).

    Kwa kuangalia uzoefu wa makada wa chama cha Umma, wengi wao wakiwa wamepatiwa mafunzo Cuba na Misri iliyoongozwa na Nasser, tunachunguza nini kilichotokea wakati wa mapinduzi yenyewe, vipi waliyalinda kwa kuziteka asasi za dola, na vipi kule kuwepo kwao (miongoni mwao si kama walikuwemo Waarabu wengi tu bali walikuwemo Waafrika na Wahindi vile vile) kulizuia machafuko dhidi ya Waarabu kuwa ndiyo madhumuni ya`mapinduzi.

    Palikuwepo na machafuko kila mahali, kama anavyokumbuka Hashil Seif Hashil, aliyekuwa mjumbe wa Kamati Kuu ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Umma (Umma Youth): ‘Watu wengi hawakujua walilokuwa wakilifanya. Jambo moja ambalo Chama cha Umma Party kilifanya lilikuwa ni kuelezea juu ya madhumuni ya mapinduzi – madhumuni yake hayakuwa kuua, kubaka au kuiba bali ni kuibadili nchi. Baadhi ya watu walielewa lakini ni wazi kuwa si kila mtu aliyeelewa’ (imenukuliwa kutoka Wilson, 1989: 12).

    Kwa mtazamo wa makada wa Chama cha Umma Party, tunakiangalia vile vile kipindi cha baada ya mapinduzi, kuundwa kwa serikali mpya ya kimapinduzi ya ushirikiano kati ya Chama cha Umma Party na Chama cha Afro-Shirazi (ASP), chama kilichokuwa kimezongwa na migogoro, na miezi mitatu iliyofuatia ambayo ilimalizika kwa vitimbi dhidi ya mapinduzi. Katika kipindi hiki, chini kwa chini, Marekani na Uingereza walipanga kuivamia Zanzibar, walikula njama kumwua Babu, na walifanya kila waliloliweza kuleta mgawanyiko ndani ya serikali mpya. Mgogoro uliojitokeza ndani ya serikali ya kimapinduzi ulisababisha kuvunjwa kwa Chama cha Umma Party, lakini makada wake waliendelea kuwa pamoja na kushirikiana katika mambo mengi wakiwa kama ni kundi moja.

    Marekani na Uingereza, hatimaye walifanikiwa ‘kuidhibiti’ Zanzibar na kuivuruga ari yake ya kimaendeleo kwa kuchochea muungano wa Zanzibar na Tanganyika ili kuunda nchi mpya, Tanzania, na raisi wake akiwa ni mtu wanaeweza kumwamini na mfuasi wa nchi za magharibi, Nyerere. Ni muungano uliopatikana kwa njia za hila, bila kufuata taratibu za kisheria zinazokubalika na bila ya kuwashauri wananchi wa nchi yoyote kati ya nchi mbili hizo. Ulianzishwa kwa njama za viongozi wanaopendelea nchi za magharibi wa Tanganyika, Kenya na Uganda.

    Hali ya Zanzibar iliporomoka hususan baada ya muungano, na Karume, kiongozi wa ASP alianza kuvitawala visiwa hivyo kama kwamba visiwa hivyo ni mali yake binafsi, akiua, akitesa na kuwafunga gerezani wote wale wasiokubaliana na sera zake na kumpinga. Tunaiangalia miaka hii ya mateso kufuatana na masahibu yaliyowafika baadhi ya makada wa Chama cha Umma Party – wale waliofungwa gerezani na kuteswa Zanzibar na halikadhalika Bara.

    Muungano uliandaliwa na kutekelezwa kwa siri lakini kwa kiasi kikubwa mchakato wa kuundwa kwake uliratibiwa kwa makini na Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, ambao nyaraka zao zimefichua sio kiasi cha dharau ya Wamarekani kwa viongozi wa Afrika tu bali pia kiwango cha uongo na ufidhuli wao. Si kama walipanga mauaji tu lakini vile vile waliwahonga na kuwajenga watu kama Nyerere ambao waliweza kuwadhibiti. Kwa mfano, mwezi Januari 1964, siku nane tu baada ya mapinduzi, G. Mennen Williams, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anayeshughulikia Afrika ya Mashariki, katika waraka wa siri, alimweleza Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, ‘Kazi yetu kubwa ni kumjenga Nyerere …. Nyerere atahitaji vitu fulani vya mpango mpya ili kuimarisha madaraka yake’ (nukuu kutoka kwa Wilson, 1989:27).

    Hivyo ndivyo hofu ilivyokuwa imetanda katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani kufuatia mapinduzi katika visiwa hivi vidogo, kiasi kwamba mnamo wiki chache tu Marekani ilimpeleka Zanzibar mmoja wa majasusi wake mwenye uzoefu mkubwa kutoka Shirika la Ujasusi la Marekani, Frank Carlucci, ambaye baadae alikuwa Waziri wa Ulinzi katika Serikali ya Ronald Reagan. Aliwasili moja kwa moja kutoka Kongo ambako Shirika la Ujasusi la Marekani lilikuwa limehusika sana katika kumpindua Lumumba. Kwa maneno ya Carlucci mwenyewe, Marekani ilibidi iwadhibiti waumini wa usoshalisti wa Zanzibar kwasababu ‘kama usingelikuwepo muungano, Zanzibar ingelikuwa Cuba ya Afrika na kutoka Zanzibar uasi ungelienea Bara zima’ (Imenukuliwa kutoka katika Wilson, 1987). Kwa kufuata ile sera iliyokuwepo kabla ya sera ya hivi sasa ya Kikosi cha Marekani katika Afrika (AFRICOM), Marekani ilianza kuandaa ule mkakati ulioitwa ‘eneo la udhibiti’ ambao ndani yake Afrika ya Kati na Afrika ya Mashariki (pamoja na Zanzibar) zingewekwa chini ya udhibiti wake, ili kuzuia ushawishi wa kisoshalisti kutoka Afrika ya Kaskazini usizifikie nchi za Kusini mwa Afrika na kuhatarisha rasilimali zao zilizowekezwa na nchi za magharibi.

    Nyaraka zilizowekwa bayana za mawasiliano ya simu za upepo za Marekani na hati za serikali ya Uingereza kuanzia miaka ya 1960 na zile za miaka michache iliyopita zilizofichuliwa na Wikileaks zinaonyesha namna fulani ya mwendelezo na tofauti zake. Kuna aina ile ile ya mfululizo wa ukusanyaji wa habari za kijasusi (ila vyanzo vya hivi sasa haviishii na wanasiasa tu bali pia vinashirikisha maafisa wa kijeshi wa Tanzania na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali); ni wasiwasi ule ule kuhusu vijana, ambao katika miaka ya 1960 wamekuwa ‘wakifanya mazoezi na kupata mafunzo kwa kile kinachoweza kuelezwa kuwa mafunzo ya ushujaa wa kijeshi’ (HMSO, 1961: 3) na hivi sasa, kwa mujibu wa simu za upepo za Marekani, wanahusika na ‘kelele za hasira’ ‘zinazohitaji kuangaliwa kwa makini’ (Ubalozi wa Marekani, 2006b) na hofu ni ile ile ya Zanzibar kuwa sehemu ya mtandao wa maadui wa Marekani. Ila sasa mazimwi ni tofauti; wakati kwanza huko nyuma walikuwa Wakomunisti, sasa ni ‘Magaidi wa Kiislamu’.

    Hebu linganisha, kwa mfano maelezo ya Carlucci yaliyopo hapo juu na wasiwasi huu wa Ubalozi wa Marekani uliopo Dar es Salaam, uliomo katika waraka wa siri wa kisera wa mwezi Julai 2008.

    Wazanzibari ni miongoni mwa wanachama wa al-Qaeda (sic) waliohusika na mashambulizi ya ubalozi huu mwaka 1998. Kuna vikundi vya wanaowaunga mkono wenye siasa kali katika kanda yote ya utamaduni wa Mswahili (mwambao wa Kenya na Tanzania, Zanzibar na visiwa vya Ngazija vyenye kuzungumza Lugha ya Kiswahili). Kundi la vijana wa Kiislamu wasiokuwa na kazi, waliokata tamaa, wasio na matumaini yoyote, walio na hasira, waliotengwa, ambao magaidi wanaweza kuwaandikisha wawe miongoni mwao ni kubwa zaidi Zanzibar kuliko mahali pengine popote katika eneo la utamaduni wa Mswahili. Mahusiano ya kifamilia na ya kibiashara katika eneo la Waswahili ni ya namna ambayo, matokeo ya jambo lolote katika sehemu moja huwagusa wa sehemu nyengine katika eneo hilo. Kuongezeka kwa watu wenye siasa kali Zanzibar kutawaambukiza watu wa eneo lote.  (Ubalozi wa Marekani, 2008a)

    Taswira ya vita baridi ilimaanisha kuwa Marekani iliamini kwamba China, au ‘Chicoms’ kama Wamarekani walivyowaita Wachina, ilihusika na kila mabadiliko ya hali ya hewa.

    China ya wakati huo ilikuwa ni nchi tofauti sana na ilivyo hivi sasa. Ilitoa ilhamu na kuwa mfano kwa nchi zilizokuwa zikiendesha mapambano dhidi ya ukoloni

    Enjoying the preview?
    Page 1 of 1