Machozi Yamenishiya
()
About this ebook
Related to Machozi Yamenishiya
Related ebooks
Kale ya Washairi wa Pemba: Kamange na Sarahani Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKielezo cha Fasili Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMashairi Rahisi:Mazoezi Na Majibu Kielelezo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNajisikia Kuua Tena Rating: 5 out of 5 stars5/5Tungo Zetu: Msingi wa Mashairi na Tungo Nyinginezo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMwana-Adam ni Nani Naye ni Nini Mungu Amkomboe: Chuo cha Kwanza, #1 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMilenia ya Kristo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsPenzi la Damu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsTishio la Ukombozi: Ubeberu na Mapinduzi Zanzibar Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsFasihi Simulizi: Kwa Shule Za Sekondari Rating: 3 out of 5 stars3/5Kufa na Kupona Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsUtatu Mtakatifu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKielezi Cha Tungo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNyuma Ya Pazia Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMfalme - Nilipumzika: Mashairi Ya Kisasa - Modern Swahili Poetry Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMvungu Mkeka Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMmeza Fupa Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsSikitiko Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMafundisho ya Utajiri Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKikosi cha Kisasi Rating: 2 out of 5 stars2/5Ufufuo & Uchukuo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsManeno na Aina za Maneno Rating: 5 out of 5 stars5/5Kionjo cha Uchokozi Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsPopote Ulipo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMiaka Miwili Ya Urais Wa Magufuli: Safari Ya Matumaini Au Nyota Iliyofifia? Rating: 1 out of 5 stars1/5Mafundisho ya Ndoa Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsJino Kwa Jino Rating: 4 out of 5 stars4/5Jinsi ya Kusali & Kuongea na Yahweh Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsZambada na Hadithi zingine Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsDunia Ina Mema Mengi Rating: 0 out of 5 stars0 ratings
Related categories
Reviews for Machozi Yamenishiya
0 ratings0 reviews
Book preview
Machozi Yamenishiya - Khelef Ghassani
NENO LA SHUKRANI
Wakati fulani mnamo mwanzoni mwa miaka ya 2000, kaka yangu, Maalim Said Suleiman, aliniuliza ikiwa tungo nilizokuwa nimeshaziandika hadi wakati huo, zilikuwa zimeshapata mchapishaji. Wakati huo ilikuwa miaka kama mitano hivi tangu alipokuwa amenitembelea nyumbani kwetu kisiwani Pemba, akiwa ndio kwanza ametokea masomoni Uhispania, na nikamkabidhi baadhi ya mashairi ambayo hadi hapo nilikuwa nimeshayaandika.
Kwenye mazungumzo hayo, nilimueleza jitihada ambazo nilikuwa nimechukuwa bila mafanikio. Nilimuambia ugunduzi wangu kuwa niliwaona wachapishaji wengi niliokuwa nimewasiliana wakiwa hawana imani na sanaa ya ushairi kwa kuwa haikuwa na wanunuzi. Mchapishaji ni mfanyabiashara na anaogopa kuwekeza kwa kisichokuwa na soko la uhakika. Tangu hapo, utamaduni wa kujisomea ni wa chini kwenye jamii zetu, na linapokuja suala la ushairi ndipo hali inazidi kuwa mbaya. Ukiwacha wanafunzi wa skuli na vyuo, ambao wanalazimishwa na mitaala yao kusoma ushairi, na ambao ni soko lililokwishamilikiwa na washairi
maalum wenye majina na au ushawishi kwa watunga mitaala, mchapishaji hawezi kuwekeza kwenye kazi ya mshairi mdogo kama mimi, akikhofia kucheza pesa zake pata-potea.
Ndipo akanishauri nimtafute Profesa Said Ahmed Mohamed kumtaka ushauri. Hilo lilikuwa ni jina kubwa sana kwangu. Sikuwa nimewahi kumuona kwa sura wala hata kufikiria kuwa kuna siku pangekuja kuwa na njia au sababu ya kukutana naye. Nikamuambia hiyo kazi angenifanyia yeye, maana sikuwahi hata kuwaza kuwa ningemfika Profesa Said wa Asali Chungu, wa Kivuli Kinaishi, wa Dunia Mti Mkavu, wa Tata za Asumini, wa Si Shetani Si Wazimu... na wa... Alimradi utetezi wangu ulikuwa ni mwingi sana, nikimuonesha kaka yangu kuwa sikuwa na pa kuanzia kumvaa
Profesa Said.
Lakini kadiri nilivyoonesha ugumu niliouhisi upo, ndivyo kaka yangu naye aliponionesha hoja na haja ya mimi mwenyewe kumtafuta mtu wa kunisaidia. Akanipa anwani yake ya barua-pepe na kuniwachia mwenyewe kufanya ninachopaswa kufanya. Naam, nikamtafuta kweli Prof. Said na nikamuomba mambo mawili: kwanza, awe mhariri wa kazi zangu za fasihi (zikiwemo hadithi fupi fupi) na, pili, atumie uzoefu wake kwenye uwanja huu kunitafutia wachapishaji.
Ajabu ni kuwa sio tu kwamba alizichukuwa kazi hizo moja kwa moja, bali pia alianza kuzitangaza kwa kila aliyemuona kuwa anaweza kusikiliza na, matokeo yake, tangu wakati huo akaniweka kwenye orodha ya waandishi na washairi wanaoinukia. Hadithi zangu fupi fupi zimekuwa zikichapishwa kwenye mikusanyiko mbalimbali inayochangiwa na waandishi wengine wachanga na wakongwe, akiwemo yeye mwenyewe, Marehemu Mohamed Said Abdullah (Bwana Msa), Prof. Ken Walibora na Marehemu Omar Babu (Abu Marjan), nikiwataja wachache. Si hilo tu, bali pia akawa ananishajiisha kila mara niandike nyengine.
Kwa diwani hii ya Machozi Yamenishiya, ambayo aliihariri na kuikamilishia kazi zake zote tangu mwaka 2007, alinifanyia la ziada jengine. Alimpa na kumuomba gwiji mwengine wa lugha na fasihi, Bwana Abdilatif Abdalla, aiwekee neno la awali. Ilikuwa sadfa yenye maana kubwa kwangu, maana hakika mimi mwenyewe ni mmoja wa wengi walioinukia kuipenda diwani ya Sauti ya Dhiki iliyoandikwa na Bwana Abdilatif na ambayo ilikuja kuniathiri sana kwenye uandishi wangu. Ni bahati mbaya kuwa Machozi Yamenishiya hayakuweza kupata mchapishaji kwa muda wote huo kutokana na sababu zile zile ambazo nimezitaja awali. Lakini ukweli ni kuwa wote wawili, Prof. Said na Bwana Abdilatif, waliihangaikia sana, hata ikafika mahala mimi – ambaye ni yangu – nikawa nawaonea huruma na kuwaambia bora waiwache tu. Haijawa riziki yangu!
Tusemavyo kikwetu. Namshukuru Mwenyezi Mungu kwamba, hatimaye, muda wa kuchapishwa umewadia baada ya zaidi ya takribani muongo mmoja wa kusubiri.
Kwa hivyo, kwa uzito wao watatu hawa niliowataja – kaka yangu, Maalim Said, Prof. Said na Bwana Abdilatif– neno hili la shukrani ni kwao. Nawashukuru kwa kujitolea kwao kwangu tangu nikiwa na umri mdogo kabisa wa kuweza kutambulika na kutambuliwa kuwa mshairi (wakati namkabidhi Maalim Said mashairi yangu kisiwani Pemba, nilikuwa na umri wa miaka 17 tu). Kikwetu, ningeliweza kusema kuwa waliniona na kunigotoa
, kwani walikuwa na jicho la ndani la kuweza kuona kuwa ndani yangu mulikuwa na kipaji kinachopaswa kuendelezwa na kupewa nafasi.
Mohammed K. Ghassani,
Agosti 2016, Bonn - Ujerumani
UTANGULIZI
MSHAIRI NA DIWANI YAKE
Linapokuja suala la kutaja mafanikio ya mshairi fulani, inatubidi kwanza tulikabili suala gumu la ki-ontolojia: ‘shairi ni nini’? Kwa vile suala hili hukosa jibu mwafaka, mimi hulipa fasili rahisi tu – yaani shairi ni umbo la sanaa-lugha linalojitofautisha na maumbo mengine ya sanaa-lugha kwa jinsi linavyosikika likisomwa kimoyomoyo au kwa kinywa kipana. Shairi, kwa hivyo, huvutia kwa utamu wake kimasikizi au kimaandishi kwa namna maneno ya kawaida yalivyoteuliwa na kupangwa kujenga hisia na kutoa taathira ya kiujumi na ujumbe.
Kwa fasili hii, shairi huwa shairi tunapokutana nalo uso kwa macho au mdomo kwa sikio, bila ya kufikiria kanuni kandamizi zinazowekwa na washairi wenyewe au wahakiki wao. Tunapolisikia au kulisoma shairi na kulifahamu bila ya kuteswa na maneno au picha