Simu Ya Kuzimuni
By Wadi Kyhia
()
About this ebook
Mengi yamasemwa na nyingi zikatolewa ahadi kwa vijana kuhusiana na mustakabali wao. Vijana wakasoma na kuhitimu, 'Someni vijana mtapata kazi nzuri sana!' Wakapiga kura kuwachagua viongozi watakaozitimiza ndoto zao, ila 'zao' zikawa ndoto zao viongozi! Wazazi, walimu na waelekezi wa vijana wayajua waingoja siku watakapoona kutimia kwa mazao ya bidii ya kuwaelimisha vijana wasomi. Nani atakayewanasua vijana kutokana na vyeti visivyozaa kazi kwenye utandu wa ufisadi, ujomba, uraibu wa mihadarati, ukabila, usorajua na maovu mengineyo?Viongozi? Labda jumuiya nyingine ya viongozi wenye azma na ari ya kuijali kesho ya vijana.
Wadi Kyhia
A trained journalist and author.I love good books.
Read more from Wadi Kyhia
Mvungu Mkeka Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKioo Chenye Kiwi Rating: 0 out of 5 stars0 ratings
Related to Simu Ya Kuzimuni
Related ebooks
Vachayeri va mbhongholo Rating: 5 out of 5 stars5/5Mmeza Fupa Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKijana Aliyetaka Afe Vizuri Na Hadithi Zingine Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKionjo cha Uchokozi Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMwongozo wa Tumbo Lisiloshiba na Hadithi Nyinginge Rating: 5 out of 5 stars5/5Zambada na Hadithi zingine Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNyuma Ya Pazia Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHatima ya Vibwengo 4: Filimbi ya Kichawi Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsSikitiko Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsPenzi la Damu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsUandishi wa Insha na Tungo Nzuri Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsTutarudi na Roho Zetu? Rating: 5 out of 5 stars5/5Mwongozo wa Kigogo: Maswali na Majibu Rating: 3 out of 5 stars3/5Najisikia Kuua Tena Rating: 5 out of 5 stars5/5Hadıısı 40 Ez’abaana N’emboozı Ezıgenderako Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHatima ya Vibwengo 2: Moyo wa Jabali Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsBahati Alikata Kiu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNsungi: NSUNGI, #1 Rating: 5 out of 5 stars5/5Mfalme - Nilipumzika: Mashairi Ya Kisasa - Modern Swahili Poetry Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsTarishi Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsJino Kwa Jino Rating: 4 out of 5 stars4/5Popote Ulipo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsSiri Kali Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsPesa Zako Zinanuka Rating: 5 out of 5 stars5/5MAISHA ya MJUSI na BUIBUI Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsSalamu Kutoka Kuzimu Rating: 4 out of 5 stars4/5Machinga mimi Masikini Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMachozi Yamenishiya Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMashairi Rahisi:Mazoezi Na Majibu Kielelezo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsDunia Ina Mema Mengi Rating: 0 out of 5 stars0 ratings
Reviews for Simu Ya Kuzimuni
0 ratings0 reviews
Book preview
Simu Ya Kuzimuni - Wadi Kyhia
Simu Ya Kuzimuni
Wadi Kyhia
Copyright 2020, Wadi Kyhia
Smashwords Edition
No part of this work may be reproduced or transmitted in any form or by any means, electronic or mechanical, including photocopying and recording, or by any information storage or retrieval system without the prior written permission of the author.
Tamthilia hii ni masimulizi ya kubuni. Majina, hulka, biashara, mashirika, mahali, matukio na visa ni mazao ya jazanda ya mwandishi au yametumika kwa kubuni. Ufanano wowote kuwaelekea watu halisi, wanaoishi au waliofariki, matukio au mahali ni tukizi tu.
Kimeandikwa na kuhaririwa
Katika Kiwara cha Utunzi
Chapisho la Fanya Mwenyewe
(F. M Publications)
mailto:wadikyhia@gmail.com
This ebook is licensed for your personal enjoyment only. This ebook may not be re-sold or given away to other people. If you would like to share this book with another person, please purchase an additional copy for each recipient. If you’re reading this book and did not purchase it, or it was not purchased for your use only, then please return to your favorite ebook retailer and purchase your own copy. Thank you for respecting the hardwork of this author.
TABARUKU
Mpendwa ninangu,
Ukarimu wa maskini hupotelea moyoni mithili ya umande jua liwakapo.Tutampaa samaki siku moja, hata kama atakuwa kambare na uvundo wake.
SHUKRANI
Ningependa kuzitoa shukrani zangu za dhati kwa Mola, mpaji wa vipaji, msanii mkuu wa vionekanavyo na visivyoonekana.
Pili, nawashukuru wahadhiri wangu katika Taasisi ya Mafunzo ya Mawasiliano nchini Kenya (KIMC) -Mlinipa mtego wenye chambo nijinasie samaki.Inshallah! Sitoula wali mkavu.
WAHUSIKA
Mwalimu Panda
Waridi
Mtama
Limau
Mtindi
Mumunye
Hindi
Mnazi
ONYESHO LA KWANZA
(Chumbani mwa mabati makuukuu katika mtaa wa mabanda wa Usorajua. Chumba hiki kilichogawanywa kwa msutu, kina uhaba wa vyombo; ila tu mikeka ya kulalia, vyombo vya kupikia na simu juu ya mkweche wa meza.Ni saa moja usiku.Kibahaluli kinawaka kwa uzembe.Waliokuwa kwa wakati mmoja wanafunzi wa Mwalimu Panda Zikua wanakutana kwenye makazi ya mmoja wao, Mashuke Mtama, kama ilivyo desturi yao. Hii ni baada ya siku kutwa ya kugaagaa huku na kule ili kutafuta riziki ya siku yenyewe ila pasi bahati.Gumzo lao linageuka na kuwa msutano)
TUMBA WARIDI: (Akiutoa ukoko wa usiku uliopita kwenye sufuria ndogo ya kusongea ugali. Ni zamu yake kukiandaa kilalio – ugali wa unga wa mtama kwa kisamvu) Mtama?!
MASHUKE MTAMA: (Kwa beuo) Naam Daktari Waridi!
WARIDI: Po! Nemsi za nini! Nakuulizaje, yaani ina