Siri Kali
()
About this ebook
Shida Kwisha ana kisa, “Mrembo alinijulisha kuhusu mradi wa kuwekeza. Bila kuuliza maswali mengi niliingia. Nami niliwaambia watu wengi lakini ni wachache sana walionisikiliza. ‘Mtu hana kitu, ni uwekezaji gani atakwambia na umsikilize?’ watu walinichekelea.”
Wale watu wa zamani walikuwa watu wa kawaida. Walikuwa maskini wakabadilika kiasi cha kuwa matajiri si wa kutajika tu bali wa kutisha. Walipataje utajiri? Swali hilo lilikuwa kero kwao kwa kuwa walitaka wao wawe matajiri peke yao. Kiini cha utajiri kilikuwa siri kali. Siri kali hiyo ndiyo aliyoipata mtu aliyetambua umaskini si kizalia. Akaitoa hiyo siri kali ya siri kali tano kwa watu ili kila mtu aweze kuwa tajiri. Siri kali ilikuwa, ni na itakuwa dawa ya mabadiliko. Ukiipata na uitumie utatajirika. Ukiipata lakini usiitumie utabaki maskini vivyo hivyo.
James Kemoli Amata
I am a retired secondary school teacher of Kiswahili (and Christian Religious Education) and an excited preventive healthcare marketer with Green World Health Products Company.I am a 1976 University of Nairobi Bachelor of Education [Arts (Hons)] graduate and a freelance content writer with a passion for writing and indeed I am a farmer-like author with many titles.I published my first book in 1985, by traditional publishing. I have tried self-publishing and now I am in great heat to explore E-publishing.However, I will never forget my Taaluma ya Ushairi (with Kitula King’ei) from which the publisher ate fat alone, and happens to be an E-book without my knowledge.As I do my business, I worship God in African Kenya Sabcrynnsk of Soi (Prayer and Healing) Church.
Read more from James Kemoli Amata
Simple Swahili for Beginners Series Book 1 Maamukizi (Salamu) - Salutations (Greetings) Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsDunia Ina Mema Mengi Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKionjo cha Unafiki Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsFasihi Simulizi: Kwa Shule Za Sekondari Rating: 3 out of 5 stars3/5Kionjo cha Wivu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsTuchambue Tamthilia: MSTAHIKI MEYA ya Timothy M. Arege Rating: 5 out of 5 stars5/5Maneno na Aina za Maneno Rating: 5 out of 5 stars5/5Bahati Alikata Kiu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKionjo cha Uchokozi Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMAISHA ya MJUSI na BUIBUI Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKiswahili Kibovu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKijana Aliyetaka Afe Vizuri Na Hadithi Zingine Rating: 0 out of 5 stars0 ratings
Related to Siri Kali
Related ebooks
Starehe Gharama Rating: 5 out of 5 stars5/5Mashairi Rahisi:Mazoezi Na Majibu Kielelezo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsUandishi wa Insha na Tungo Nzuri Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsBahati Alikata Kiu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNyuma Ya Pazia Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsCheka, Simulia, Lakini Usiombe Yakukute Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMafundisho ya Utajiri Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMakosa Kumi Makuu Ambayo Wachungaji Wanafanya Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsManeno na Aina za Maneno Rating: 5 out of 5 stars5/5Kale ya Washairi wa Pemba: Kamange na Sarahani Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsJinsi Ya Kupata Mme Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNjia za Utu kuelekea kwa Furaha: Hekima vitendo (Swahili Version) Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNdoa ya Mfano Wa Kuigwa Rating: 4 out of 5 stars4/5Kawaida Grace Kuokolewa kwa Makusudi Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsPeter DM Bwimbo: Mlinzi Mkuu wa Mwalimu Nyerere Rating: 5 out of 5 stars5/5Jinsi Unavyoweza Kutimiza Huduma Yako Rating: 5 out of 5 stars5/5Ujasusi Ni Nini? Na Je Majasusi Wanafanya Kazi Gani Hasa? Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMiaka Hamsini ya Kiswahili Nchini Kenya Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKijana Aliyetaka Afe Vizuri Na Hadithi Zingine Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNajisikia Kuua Tena Rating: 5 out of 5 stars5/5Nsungi 2: NSUNGI, #2.3 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsTarishi Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKifungo Cha Bikra Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMachinga mimi Masikini Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsDimbwi la Damu Rating: 3 out of 5 stars3/5Salamu Kutoka Kuzimu Rating: 4 out of 5 stars4/5Jino Kwa Jino Rating: 4 out of 5 stars4/5Popote Ulipo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMwongozo wa Tumbo Lisiloshiba na Hadithi Nyinginge Rating: 5 out of 5 stars5/5Kuku aliyegeuka kuwa Kanga Rating: 0 out of 5 stars0 ratings
Reviews for Siri Kali
0 ratings0 reviews
Book preview
Siri Kali - James Kemoli Amata
Siri Kali
Iwapo bado unaabudu uajiriwaji kazi na mtindo wa zamani wa kufanya biashara, USIKISOME KITABU HIKI.
James Kemoli Amata
Vitabu vingine vya mwandishi huyu
Mwongozo wa Kipekee wa Mwisho wa Kosa, Africawide Network
Mwongozo wa Kipekee wa Kifo Kisimani, Africawide Network
Mwongozo wa Kipekee wa Mayai Waziri wa Maradhi na Hadithi Nyingine,
Africawide Network
Mwongozo wa Kipekee wa Utengano, Africawide Network
Mtaala wa Fasihi Kwa Shule Za Sekondari, Igudwa Publishers
Highly Regretted: An autobiography of a bad teacher, AuthorHouse, 2010
Kisa cha Zahara Mage, Mvule Africa, 2008
A Villa For Zahara
An Introduction to the Theory and Practice of Network Marketing
Bahati Alikata Kiu
Before and After Your Wedding
Don’t Wait for the Government
Dunia Ina Mema Mengi
How I Became God’s Enemy
How To Fail Any Examination
Keep on scratching! Or change by choice
Kijana Aliyetaka Kufa Vizuri
Life is Health and Wealth
Mashairi Rahisi: Mazoezi na Majibu
Mitihani Kielelezo ya Kiswahili KCSE
Nelson Mandela Madiba
Obesity and Poor Health
Relax, Doctor
Satan In An Angel’s Robe Hid in Sabcrynnsk
Ushairi na Aina na Bahari za Mashairi
You Can Be There Before You Reach There
Beauty Face
Let Us Heed Good Advice
Tuchambue Tamthilia: Mstahiki Meya ya Timothy M. Arege
Sweet Beauty Face
Siri Kali
James Kemoli Amata
Anwani ya Mahali:
Tiens Specialty Shop
KVDA Plaza, Mezzanine Floor
Eldoret
Kenya
Anwani ya Posta:
PO Box 2-30105
Soy
Kenya
Rununu: +254 721 720 699/+254 734 720 699
B-Pepe: kemoli2003@yahoo.com
Siri Kali
Hakimiliki© James Kemoli Amata, Jumamosi, Septemba 08, 2012
Ni jambo la aibu na kinyume cha sheria mtu mwenye mizani kujigeuza kupe na kula jasho la mtu mwingine.
Kimetangazwa
Na James Kemoli Amata katika Smashwords, Jumatatu, Juni 03, 2013
Maelezo ya Idhini ya Toleo la Smashwords
Kitabu hiki cha kielektroniki kimeidhinishwa kwa raha na furaha yako peke yako ya kibinafsi. Usikiuze tena wala usiwape watu wengine. Ukitaka kutumia pamoja na mtu mwingine, tafadhali nunua nakala ya ziada kwa kila mtumizi. Iwapo unakisoma kitabu hiki lakini hukukinunua au hakikununuliwa kwa matumizi yako wewe peke yako, hivyo basi kirudishe kwa Smashwords.com na ununue nakala yako mwenyewe. Asante kwa kuiheshimu kazi ngumu ya mtunzi huyu.
Nawatabaruku
Rose M. Adagala, Esther Sumukwo na Jemimah Kang’alika Mwangi
Kimekokotolewa na Lilian Mumbua Odoyo
Usanii wa jalada na Edward Odoyo
Picha ya jalada ni kwa hisani ya Judy Jebichii Ng’etich
Ukiri
Bila Jeniffer Chepkirui Lihasi, wa Modern Professional Centre, Soy, singeweza kuisarifu kazi hii. Daima amekuwa msaada kwangu kila niwapo na haja ya huduma za tarakilishi.
Beatrice Amwayi wa Kogo Plaza, Eldoret, ametekeleza wajibu muhimu sana katika kuiwezesha kazi hii kuwa jinsi ilivyo.
Katika uandishi wa kitabu hiki nimewafurahikia Catherine Sarbabi, Eveleen Pwokah, C.B. Peter, Isaac Kimaiyo Chebii, Richard Wekesa na James Shimanyula.
Mkono wa Wilson Maiyo u katika kazi hii.
Nukuu
Ugali usio na kitoweo usinichome bure,
hayati Babu Mzee Musa Idah alisema.
Nitayakumbuka daima maneno hayo, hasa tangu alasiri ya Mei 25, 1999.
Siri Kali
James Kemoli Amata
* * *
Hints
Kitangulizi
1
Watu Waliokuwa Si Watu
2
Mbegu Mbaya
3
Elimu Ya Mabadiliko
4
Enzi Mpya
5
Ukweli Mchungu
6
Umaskini Si Kizalia
7
Watu Na Ndoto Zao
8
Nafasi Ya Mwisho
9
Jahazi Limeng’oa Nanga
10
Maisha Ya Kuyagura
11
Ruwaza Ya Mrembo
12
Kizazi Kipya
13
Kumbukumbu
14
Shukrani
Faharasa
Mwandishi
Kitangulizi
USIKISOME KITABU HIKI, iwapo unachukia upuuzi
Iwapo kweli unachukia upuuzi, HIKI KITABU USIKISOME!
Naomba nianze kwa shajara, hasa sehemu tu ya shajara. Jumanne, Septemba 15, 2012 tulimzika Amu Abinayo Majanga Idah.
Jumanne, Machi 19, 2013 tukamzika Shangazi Deborah Lunyagi.
Hapa ndipo sehemu tu ya shajara yangu inaanzia na hata tena si mwanzo bali ni kama kichocheo cha hadithi hii ya kubuni huku ikitishia kuwa kisa cha kweli kilichosheheni UKWELI.
Kabla ya hii siku niliota ndoto mbili na si ndoto mbili bali ni ndoto mbili tu ambazo nimechagua kwa uamuzi wa kibinafsi kuziandika katika hii sehemu tu ya shajara.
Kumbe ndoto niliyoiota haikuwa ndoto tu, ilikuwa UKWELI, ukweli mtupu.
Nilikuwa nyumbani, kijijini. Nikakuwa nimeliegesha gari langu si gari la PRADO Land Cruiser jeusi. Akaja Meya (ambaye kwa heshima zote sitamtaja jina) akashangaa na kutokwa, "Kali Mr Kemoli yagula ku umudoga kuli yigu mba (Hata Bw Kemoli hajawahi kununua gari (kubwa) kama hili), Mudanyaatulizi hayi izisendi zyagulii umudogigu (Mudanya ametoa wapi pesa ambazo amenunulia gari hili)?"
Hiyo ndoto si ndoto tu iliyopita hivyo lakini sijawahi kuisahau. Hata niliiandika pahali.
Ndoto ya pili na si hiyo tu bali ni ndoto nyingine lakini ya pili mimi kuiandika katika sehemu hii tu ya shajara.
Nilikuwa katika nyumba ya baba yangu. Nje ya nyumba yangu nilikuwa nimeegesha magari mawili mapya. Tukiwa amu yangu mmoja (ambaye kwa heshima zote sitamtaja jina), baba yangu na mimi, amu alifadhaika, "Onyoo hai izisendi zyugulii imidoga jivili (Umepata wapi pesa ambazo umenunulia magari mawili)?"
"Mbuguu ku zizyo (Nilitoa katika zako), katika hasira iliyojificha katika unyenyekevu, nilimpa jibu.
Henza mwa kaunti yoyo olole (Angalia katika akaunti yako uone)."
Basi hizo ni ndoto tu na ndoto ni ndoto tu kwa watu wengi. Sikwambii mimi ni mmoja wao au la. Wasomi husema ndoto ni mawazo aliyokuwa nayo mtu, kwa ufahamu au la si hoja. Kwamba ndoto ni matokeo ya ubongo kushughulika ama pengine kuhangaika kwa sababu ya mawazo ndio ujuba wa watu waliovila vitabu vihusuvyo utendakazi wa ubongo.
Liwalo na liwe.
Siku nyingi tangu tujuane
Marehemu Victor Malova alikuwa mtu mwema sana sana. Akiwa katika gari yao au ya rafiki yake, akiendesha au kama amebebwa, alikuwa hamwachi mtu yeyote aliyekuwa anaelekea alikokuwa anaelekea.
Noah ni mtu wa watu katika barabara hiyo.
Mwalimu Juvenalis Skipper Nyongesa amekuwa akinibeba katika gari lake. Siku moja nilimtaka msaada anipelekee watoto na wajukuu wangu hadi Soy waabiri gari kwenda Voi. Siku hiyo walikuwa wasafiri kwa Simba Coach ambayo haimgoji abiria nayo mvua ikawa inanyesha kunyesha.
Nilifunza na Grace Luvonga. Mume wake amekuwa akinibeba kutoka Soy na badala ya abetee mahali pake amekuwa akipapita anifikishe nyumbani ndipo ageuze gari kwenda kwake.
Barabara ya Likuyani-Kogo ina watu wengi wazuri sana wenye magari ya kibinafsi. Daktari Oyugi na Mzee Arthur Gitonga daima hawaniachi wanaponipata barabarani nikienda au nikitoka Soy. Pamoja na hao yupo Daktari Munala wa Seregeya ambaye siwezi kumsahau kati ya watu ambao kuwemo kwangu katika magari yao si kero. Wangekuwa wananipita kama kwamba hawajaniona. Barabara iyo hiyo ina mtumishi mmoja wa Mungu. Haikosi aliamriwa, Usiwahi kumbebea mwanadamu awaye yeyote yule katika hili gari. Utakapofanya hivyo hakika utakufa.
Kumbuka hapo atakaye kufa.
Siku moja
Nilikuwa Soy nikitaka kwenda Eldoret kwa bahati tu nikamwona David Alela. Nilimsalimia na kumwambia nilikokuwa ninaenda. Alikuwa na furaha sana kunipeleka. Sikuwa nimejua alikuwa amechomoa chuma.
Ijumaa, Machi 15, 2013
Shangazi yangu Deborah Lunyagi aliaga dunia baada ya muda mrefu wa kuugua ugonjwa wa shinikizo la damu na ndugu yawo kisukari.
Maziko yalikuwa Jumanne, Machi 19. Baba alitoka nyumbani, akiandamana na mzee wa kijiji Mugera, mbele yangu. Punde tu nikawa nimekaribia kufika katika njia ya kwenda Mwilongo, hadi Bendera. Akatokea Kidaha katika gari lake. Aliangalia nilikokuwa. Punde tu nilifika barabarani nikawa ninakimbia niwafikie baba na mzee wa kijiji. Nikaona wanaabiri gari la Kidaha. Nilijongea katikati ya barabara ikawa hawangeniona katika kioo cha kando. Wakaondoka wakaenda. Punde bodaboda wa pikipiki alifika nikamwuliza anipeleke hadi makutano ya Chavakali.
Kufika Chavakali wazee waliokuwa mbele yangu walikuwa wameshuka na wanataka kuabiri gari la kutupeleka Bunyore, Ivunangwe.
Ulikuwa wapi?
baba alishangaa.
"Nilikuwa tu katika gari mlimokuwa lakini hamngeniona.
Kilikuwa kicheko. Mzee wa kijiji aliponiuliza niseme ukweli nilimpa jibu fupi, "Amadiku gaa gukugingwa gafa (Siku zangu za kubebwa ziliisha), ndukanaa mbe ning’ingaa avandi (nastahili niwe nikiwabeba wengine).
Rafiki, baba na ndugu Seth Ambale alikuwepo. Sitasahau alinisisitizia, "Kilimo ni muhimu sana sana katika maendeleo. Huwezi kuendelea bila kilimo. It is very very very important." Nilichekea rohoni huku nikimjibu kimoyomoyo, ‘Mbona wakulima hawapatikani katika orodha ya Who owns Kenya au Who is who in Kenya?’
Siku iyo hiyo nilimjulisha amu William (Listwa) Idah habari moto kuhusu Levitical Investment Company Limited (LICL). Yeye ni mkulima kwa ajili ya maisha ya humu duniani mlimo mema mengi. Nitaulizia zaidi halafu nichukue uamuzi mwafaka,
alihitimisha maelezo yangu.
Jioni, Imbuga Alex, Amosi Listwa na mimi, tukawa tunarudi. Tulipofika Chavakali, karibu na NCPB ambayo ni nadra iwe na nafaka zozote, Imbuga aliona gari la Musungu (Si Musungu wa hii hadithi), ndugu yake Kidaha. Akawa mwepesi kwenda kumwuliza iwapo angetupeleka nyumbani.
Musungu akamjibu hakuwa akienda nyumbani. Tukaendelea kwa haraka tukiomba sana mvua ituhurumie tufike kwanza. Mvua ilitupata vizuri sana mara tu baada ya kuifikia lami katika kona kabla ya Bendera. Tulijikinga hapo ikanyesha mvua kubwa sana lakini tukashukuru sana kwa kuwa hatukunyeshewa.
Mvua ile ilinyesha kwa muda mrefu. Ilipokatika tuliendelea na safari yetu tukawa tumepita Mwilongo tumemaliza mlima. Musungu akatufikia akitaka kutubeba pasipo haja kwani tulikuwa tumekaribia mahali pa mimi kubetea. Kama Imbuga na Amosi wangeabiri mimi singeabiri kwani nilikuwa nimebakiza masafa mafupi tu na niwe nimefika.
Jumamosi, Aprili 13, 2013
Nilikuwa njiani natoka Likuyani naenda Soy. Nilikuwa nimefika mahali panapoitwa Kwa Rubeni. Akanifikia Prinsipo Fredrick Mwanyumba Tweni katika gari lake zuri. Alinipungia mkono wa salamu akaendelea na safari yake. Nilizifurahia sana salamu zake ambavyo si kawaida watu wawasalimie wenzao siku hizi wazisemazo ni za shughuli nyingi na za kung’ang’ana daima dawamu. Hawana furaha ya salamu na hawana nafasi ya salamu. Nilipofika Home Cup, mahali ambapo barabara imeoza kuoza na hata haipo, paombewapo, Magari yakwame tusukume tule kitu,
alinifikia Fredrick Simiyu katika pikipiki yake. Akasimamisha pikipiki yake na kunisalimia. Nikamtaka aendelee na safari yake akanijibu, Siwezi kukuacha na unatembea ukienda kule ninakokwenda.
Niiifurahia lifti kwa kuwa mtu akikupa lifti anakuokolea muda fulani tukielewa muda si kama pesa ambazo ukigawana na watu unasifiwa lakini ukigawana muda wako na watu unaonekana kama mtu ambaye hana kitu muhimu cha kufanya.
Jioni nilipokuwa nimefika Kwa Rubeni ninarudi baada ya shughuli zangu niliona mtu katika Prado yake akimrushia bodaboda wa pikipiki maji ya matope shwaaaaaa!
Jumatano, Aprili 17, 2013
Jioni, mke wangu akitoka kanisani alikutana na rafiki yangu Pasta John Ombodo. Akawa na jambo kwake. "Msalimie rafiki yangu. Huwa tunakutania Eldoret. Alinipeleka pahali katika kitu Levitical. Margaret, anoho kogotaa (Margaret, ama tunapotea)?"
La hasha, m sawasawa,
akampa moyo bila kusita. Hamjapotea hata kidogo, mtakuja kuhisi raha hapo baadaye.
Maneno haya ni hisia za watu wengi. Mungu abariki.
Alhamisi, Aprili 18, 2013
Kuna uwezekano tunashindwa kuwavutia watu na kuwashawishi kwa namna tunavyowakabili na kuwasiliana nao. Nilikuwa njiani naenda Soy. Akanifikia mtu mmoja wa bodaboda ya pikipiki. Mzee huna hata za chai mfukoni?
Nini?
Huna hata pesa kidogo tu za chai yangu?
Mtu akikuona unatembea yupo yule ambaye mara moja anajua huna pesa.
Mtu akikuona unatembea yupo yule ambaye daima anajua unabania pesa.
Unaweza kuwa unatembea kwa sababu unataka kuonana na kuongea na