Hanjamu Ya Msaliti
By Mambosasa
()
About this ebook
Siku zote msaliti hakubali kuona akisalitiwa, hata kama kukiwa hakuna dalili ya kufanyiwa hivyo. Hawezi kuwa na amani asilani, daima huhisi atageukwa kama alivyogeuka mwingine. Hawezi kustahimili kufanyiwa jambo alilomfanyia mwingine, maumivu yake huyajua.
Ndiyo hapo Saibah binti wa Sultan Zuad aliyemsaliti mumewe, mpaka akaja kufumwa na kijakazi kitandani. Bado alifikia kumwonesha jeuri ya waziwazi na si kukubali alikosea, kisa nyumba waliyoishi ni kwao. Mpaka bwana yule aliamua kuondoka na kumwachia nyumba, na akabaki akikaa nje akiendelea na majukumu yake kama Mkuu wa majeshi wa himaya.
Aliachwa solemba na kijakazi yule, akaja kujua mume ni wa muhimu. Wakati ambao yupo vitani. Alipokuja kurudi ni majeruhi na hana fahamu, muda huo napo mwanamke aliyependwa na mumewe anarejea kumjulia hali. Ndiyo hapo sasa wasiwasi wa penzi wa msaliti unapoibuka
Mambosasa
Hassan Mambosasa born in Tanga region in Tanzania. He won Nyabola kiswahili for short stories in 2022. Currently he live in Tanga city.
Read more from Mambosasa
NSUNGI Jino Kwa Jino Rating: 4 out of 5 stars4/5
Related to Hanjamu Ya Msaliti
Related ebooks
Nsungi 2: NSUNGI, #2.1 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsPopote Ulipo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsPenzi la Damu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsZambada na Hadithi zingine Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNsungi 2: NSUNGI, #2.3 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsTutarudi na Roho Zetu? Rating: 5 out of 5 stars5/5Tarishi Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNsungi 2: NSUNGI, #2.2 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNjama Rating: 5 out of 5 stars5/5Pesa Zako Zinanuka Rating: 5 out of 5 stars5/5Hatima ya Vibwengo 4: Filimbi ya Kichawi Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMtambo wa Mauti Rating: 5 out of 5 stars5/5Kufa na Kupona Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsSiri ya Sala Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHisia ya Hatia Ichomayo - Sura ya 5 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNajisikia Kuua Tena Rating: 5 out of 5 stars5/5Nyuma Ya Pazia Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKufikirika Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNsungi: NSUNGI, #1 Rating: 5 out of 5 stars5/5Mvungu Mkeka Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMmeza Fupa Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHatima ya Vibwengo 1: Wanajeshi Shupavu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNyuma ya Mapazia Rating: 5 out of 5 stars5/5Kuku aliyegeuka kuwa Kanga Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKielezo cha Fasili Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKifungo Cha Bikra Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMungu Nisaidie Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKurejea kwa Malkia Nkamba wa Nyakayenze Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsSalamu Kutoka Kuzimu Rating: 4 out of 5 stars4/5Densi Ya Mwezi: Mfululizo Wa Vitabu Vya Kuunganishwa Kwa Damu Kitabu Cha 1 Rating: 0 out of 5 stars0 ratings
Related categories
Reviews for Hanjamu Ya Msaliti
0 ratings0 reviews
Book preview
Hanjamu Ya Msaliti - Mambosasa
DIBAJI
Sultan Zuad, mtawala wa himaya anaumizwa kichwa na kuhusiana na binti yake. Ameshafikisha umri ambao anauona unatosha kuolewa, ila bado binti hana uelekeo wa kutaka kuolewa. Wachilia mbali kumpata huyo mchumba wa kumchumbia, suala ambalo si kawaida kwenye himaya hiyo.
Kawaida ya tawala za enzi, binti wa kufikia umri huo alitakiwa kuwa kaolewa au tayari kachumbiwa. Ndiyo hapo sasa Sultana anafikia kumweleza mkewe kuhusiana na suala hilo. Naye anaenda kumfikishia binti yao, ambaye aliishia kusema waitwe vijana wa mji mzima atachagua yupi ambaye angemfaa kuwa mumewe. Suala hilo linatimizwa.
Fuad kijana wa kuzaliwa baba mwarabu, na mama mweusi anafanikiwa kumwokoa waziri wa serikali ya Sultan, aliyekuwa akizama baharini. Jambo ambalo linalazimu kufanyika kwa karamu, na kupongezwa kwa jambo hilo. Kwa kijana wa kimasikini kujipa ushujaa huo ambao hata magadi wa waziri yule hawakuweza kuufanya..
Upande wa binti Sultan kweli alifanikiwa kuendesha shindano hilo la kumsaka mume. Ila hadi linamalizika hakumpata aliyemtaka. Aliishia kutoa sababu ambayo hadi kwa mzazi wake ilikubaliwa na siku hiyo ikapita nayo.
Siku inayofuata binti anaenda sokoni kununua vitu muhimu, kwa ajili ya maandalizi ya siku ya tafrija ya kupongezwa kijana aliyemwokoa waziri. Huko napo anakutana na Fuad dukani, ambaye alikuwa akilalamika apewe pesa yake na muuzaji, ndiyo hapo aje kupisha binti wa sultan aingie kununua.
Binti anaishia kumwamuru mtumishi wake amuumiza, na anaondolewa dukani hapo akiwa na jeraha mguuni. Mchana nao unapita na hadi unakuja kufika wakati maalum wa kupongezwa kijana kwa kumwokoa waziri.
Binti Sultan anakutana na kijana tena kwa mwonekano mwingine. Anaonekana kuvutiwa naye ila napo anajikuta na wakati mgumu, baada ya kuambiwa waziwazi aliyemdharau mchana wa siku hiyo ndiye huyohuyo.
Inakuwa zamu yake kuanza kuhangaika, hasa baada ya kuona mambo kadhaa yaliyomvutia mno kwa kijana huyo. Ila napo Fuad hana shida naye, wala mali za nyumbani kwao. Inamuwia vigumu sana kumpata.
Fuad ana mpenzi anayeitwa Semeni, ambaye anampenda hasa. Ila napo binti anaingiwa na wakatii mgumu. Ikiwemo kupokea vitisho yeye na familia yake, inambidi kuondoka mbali hasa wakati huo kijana ni mwenye maisha mazuri sana kutokana na zawadi nzuri alizopewa ikiwemo nyumba na eneo.
Ndiyo kwa wakati huo binti Sultan anapohimiza sana kwa baba yake amsaidie aolewe na Fuad. Sultan kwa kumpenda bintiye anaenda kumshawishi, mwishowe anakubali kwa heshima ya kiongozi huyo na si kwamba alimpenda mtoto wake. Anaozwa na kutokana na uwezo wake kivita aliyobainika nao anaingizwa na jeshi na kufanywa mkuu wa majeshi.
Furaha ya ndoa yao napo haidumu, binti anamchoka mumewe mapema. Anakuja kurudisha penzi la siri sana, alilokuwa akilifanya na mtumwa wake. Kumbe hata usichana wenyewe haukuwa nao hadi muda wa kuozwa. Ila mumewe aliamua kumhifadhi hakusema kitu. Mwishowe anakuja kumrudisha aliyemwanza kwa usiri.
Mwishowe wanakuja kufumaniwa ila bado binti anajawa na kiburi, akamtakia maneno mabaya ikiwemo kuishi kwenye nyumba ambayo ni mali yao. Ndiyo hapo Fuad alichukua hatua ya kuondoka zake, ila napo binti anakuja kuachwa ghafla na yule kijakazi. Kumbukumbu za mume zinamjia, anajijua anamhitaji hasa. Alipomwita anabaini ameshaondoka vitani, hayupo mjini.
Fuad anakuja kurudishwa mgonjwa kutokana na kujeruhiwa na upanga wenye sumu. Semeni naye ambaye ana maisha mazuri, alirejea upesi sana baada ya kuipokea habari hiyo. Hapo ndiyo mtihani unatokea, msaliti alipohisi atasalitiwa na hataki hilo litokee.
1
Mvumo wa kutoka mashariki kuelekea magharibi ulirindima, minazi pamoja na miti mingine iliyopo ndani ya mandhari hiyo. Ilipepesuka vibaya kwa mkumbo huo, hali hiyo ilidumu ikiwa na karaha kubwa kwa miti ambayo haikuisha kulalama ikitoa mivumo ya aina yake pale matawi au makuti yalipovamiwa. Karaha kwa viumbe hai waliyojichimbia ardhini, ikawa ni burudani kwa viumbe hai watembeao juu ya mgongo wa ardhi. Mgeuko wa hali ya hewa kutoka ile ya joto liletwalo na jua hadi kuwa mpulizo, ndiyo ikawa hivyo kwa upande wao.
Wakati huu eneo la kiwambaza cha juu kabisa la kasri la kifahari, alionekana Mtu mzima mwenye kilemba chenye taji kichwani mwake. Kanzu matata ya rangi ya kahawia ikiwa imemkaa mwilini mwake, miguuni akiwa amevaa kiatu kilichoinuka mbele mithili ya pembe la Ng'ombe. Huyu alisimama akiwa ameweka mikono kwenye ruva za sehemu hiyo ya juu, kando yake kukiwa na vijana wawili waliyoshikilia magobori. Macho yake aliyaelekeza mbele hatua takribani mia moja ambapo kuna ufukwe wa bahari ukiwa na bandari iliyoegeshwa Majahazi kadhaa.
Alijidhihirisha ni namna gani alivyozama ndani ya dimbwi la fikra, hata pale kiumbe mwingine alipofika hapo na kumwita. Hakuweza kung'amua hilo, kama vile ni mwenye kutosikia. Kumbe wala haikuwa hivyo, isipokuwa kuwa mbali kinafisi ikapelekea hayo. Aling'amua kuwa anahitajika na yule aliyepo nyuma yake, hadi pale alipoguswa begani na kiganja ndiyo akageuka nyuma kutazama.
Muhibu lipi likusibulo maana wananitia shaka kupitiliza
Aliambiwa na Mwanamke mwenye mavazi ya gharama mwenye taji kichwani mwake, hapo akajikuta mwenyewe akiinama chini kwa sekunde kadhaa baada ya kuulizwa hivyo.
Mahbuba, hababi wa fuadi wangu. Mwenye kuisuuza roho yangu, unayependezwa na mtima wangu. Kipi kikusibucho?
, Aliulizwa kwa mara ya pili.
"Ewe Malkia wangu, mtawala wa moyo wangu. Sina kingine ila isipokuwa ni hili la Saibah. Wajua umri unakwenda na sasa umri wake kafikisha eshwiriin, wala haoneshi dhumuni la kutaka Shababi. Yaa Habib ninaihofu fedheha kuliko kitu kingine chochote juu ya Binti yangu, kukaa bila ya mume mtoto wa Sultan Zuad", Alieleza
Ni haki yako kuwa namna hiyo ya Habib, ila binti mwenyewe nadhani wamwona. Hasikii wala haeleweki ni kipi akifiriacho juu ya hilo, hata mimi naapa kwa jina la Allah sipo tayari kuona ninapatwa na fedheha kisa yeye
Hakika wewe ni mama mwema kwa binti yako, basi ni wajibu wako kuongea naye juu ya suala hili. Kama ni kitabu basi wanazuoni kadhaa amepitia na amehitimu mapema kuliko wenzake, je lipi hilo alisubirilo. Laiti kama ingelikuwa Makuhani si haramu kisharia, basi ningaliwafuata na kuhitaji jua tatizo la binti yangu
"Afuan yaa Muhibu, madhali limefika kwangu nitakaa niongee naye juu ya hili. Na imani katu hawezi kuniangusha mimi mamaye"
Haswaaa! Mama bora haangushwi na bintiye
Huu ni mguu niuinuao hivi sasa ni wa kwake, nikatete naye juu ya suala hili
Malkia aliposema hivyo, alimwacha Sultan Zuad akiwa yu pekee yake mahali hapo. Ahueni ilianza kuonekana usoni mwake, baada ya kuhakikishiwa hilo suala na mkewe. Alianza kujihisi ni mwenye aibu kuu kwa kukaa na binti muda mrefu ambaye hakuozwa, fedheha alihisi angeweza kuiepuka majira yeyote yale baada ya kupokelewa vyema na mkewe kwa taarifa hiyo.
Aliendelea kuwepo eneo hilo akibarizi upepo mwanana wa bahari, alikaa hapo kupunguza joto lakini kipunguzo kilipozidi kiwango. Aliamua kugeuka nyuma na kurejea ndani, majira hayo ni ambayo hali ya hewa ya baharini ilibadilika ghafla na wingu likatanda kila pande. Kuhofia kushuka kwa mvua akiwa ambapo huweza kumpata ikiwa itanyesha ile ya kiupande, ambayo huweza kumpata ingawa sehemu ya juu imeezekwa.
Kuingia kwake ndani hakukuonekana mabadiliko yeyote ya hali hiyo ya mawingu mazito, isipokuwa ni upepo mkali ukiendelea kuvuma.
JUA KUONDOKA GHAFLA na ujio wa upepo mkali pamoja na mawingu mazito, ulipelekea hata mawimbi ya bahari nayo yabadilike ukubwa na kuwa ya kutisha. Yalifika umbali mkubwa tofauti na pale ambapo hufikia nchi kavu. Hakika watu walielewa wazi chanzo hicho kikubwa cha maji kuliko vyote duniani, kimetibuka na wale waliyokuwa wana vyombo vidogo vya uvuvi. Hawakuthubutu kuingia huko, kuhofia kukumbwa na dhoruba kali zaidi wakiwa wapo majini.
Upande wa katikati, eneo la mbali kutoka ilipo fukwe. Vijana wenye rika tofauti walionekana wakishindana nguvu na mawimbi makubwa. Mashua yao yalipelekwa kutoka upande mmoja kwenda mwingine, huku maji yakiingia ndani na kuzidi kuleta athari kubwa kwao. Iliwabidi wafanye kazi ya ziada kuweza kujinasua ndani ya kibweka hicho. Vyombo vya kuchota maji pamoja na ulindwaji wa mizigo yao, waliufanya majira yote wakiwa wanaelekea ufukweni.
Kakweree! Shikilia kamba hiyo ya Tanga!
, Kijana mmojawapo aliyekaa nyuma akiwa amejishikilia mkono wake kwenye ukingo wa Mashua alipaza sauti.
Kabwariii! Endelea kuchota maji hivyohivyo jamani, huu mzigo wa leo ni mkubwa kupitiliza. Tuhakikishe wafika ufukweni
, Alimhimiza mwingine huku yeye akiiinama chini kwa haraka baada ya tanga kuzunguka kwa ghafla na kufanya mashua yao yabadili mwelekeo.
Turudishe tanga mahali pake, hakuna kukata tamaa
, Aliwahimiza na safari hii akiwa wa kwanza kulishika, wenzake nao walifuatia na kulirejesha lilivyokuwa hapo awali.
Kutoa maji chomboni na kumwaga nje, kulidumu na hakuna aliyeonesha dalili ya kuchoka. Daima hiyo ni moja ya changamoto ya kufanya kazi baharini, kukabiliana nayo ni wajibu na si kuikimbia. Ndiyo maana hawa hawakutaka kurudi nyuma kwenye suala hilo, waliendelea kugangamala nayo
Wakiendelea hivyo, hatimaye waliweza kufika mahala ufukwe wanauona kwa mbali. Hapo ndipo walizidisha juhudi zaidi hadi wakafanikiwa kufika ufukweni salama, Mashua yao waliyafunga kwa kamba ngumu kisha wakaanza mara moja kazi ya kutoa mzigo pasipo kujali ukubwa wa mawimbi yanayojiri. Kwa uwezo wake Jalali, aliyowajalia