Roho Mtakatifu
By Ninah Shali
()
About this ebook
Kwa mtu anayesoma ujumbe huu, wewe ni muhimu sana kwa Mungu na ulimwengu mzima. Je, inaonekana kana kwamba chochote unachofanya maishani, huwezi kupata matokeo unayotaka? Je, unatafuta majibu katika sehemu mbalimbali za maisha yako? Inaweza kuwa ya kiroho, kihisia, kisaikolojia, kijamii, kiuchumi, kitaaluma au afya.
Unaposoma kitabu hiki, amini kwamba utatambua suluhu la kudumu kwa(za) changamoto zako kwa usaidizi wa nguvu kuu zaidi, nguvu za Roho Mtakatifu. Kitabu hiki kitakuwezesha kupata furaha, amani, na uwezo wa kushawishi na kubadilisha mapenzi yako, kukidhi hitaji lako kuu na kuanza kuishi maisha yenye mafanikio.
Unaposoma kitabu hiki, Roho Mtakatifu na awe halisi kwako kama ambavyo amekuwa kwangu kwa miaka mingi hadi sasa. Kuanzia sasa, tembea katika ushirika wa ndani zaidi na Roho Mtakatifu. Shalom.
Related to Roho Mtakatifu
Related ebooks
Waambie Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHatua za Ukuaji wa Kiroho Rating: 4 out of 5 stars4/5Siri ya Kifo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsJivutie Upako Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsUanzishaji Wa Imani: Taasisi ya mafunzo ya Isaya 58 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsGUNDUA UCHUKUZI WAKO Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsItaje! Idai!! Ichukue!!! Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMguso Mzuri Wa Upako Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsJinsi Ya Kuzaliwa Mara Ya Pili na Kukwepa Kuzimu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsEneza Huduma Yako Kwa Miujiza na Udhihirishaji wa Roho Mtakatifu Rating: 4 out of 5 stars4/5Ukweli Muhimu Kwa Ajili Ya Waumini Wapya Rating: 3 out of 5 stars3/5Katika Eneo la Adui Kuokolewa na Silaha ya Siri: Swahili Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWaitwao ni Wengi Rating: 4 out of 5 stars4/5Ujio wa Pili wa Yesu Kristo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHow To Hear From God - SWAHILI EDITION: School of the Holy Spirit Series 7 of 12, Stage 1 of 3 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHistoria & Maisha ya Yeshua Kristo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHere comes A Day of Darkness - SWAHILI EDITION: School of the Holy Spirit Series 9 of 12, Stage 1 of 3 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsUtatu Mtakatifu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMpakwa Mafuta na Upako Wake Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsUfufuo & Uchukuo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMwongozi Wa Roho: Safari Maishani Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsSoma Biblia Yako, Omba Kila Siku ...Ukitaka kukua Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMafundisho ya Ndoa Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMwana-Adam ni Nani Naye ni Nini Mungu Amkomboe: Chuo cha Kwanza, #1 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsJinsi ya Kusali & Kuongea na Yahweh Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMafundisho ya Utajiri Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMilenia ya Kristo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMahubiri juu ya Mwanzo (III) - Hakuna Machafuko zaidi, Utupu au Giza Sasa (I) Rating: 0 out of 5 stars0 ratings
Reviews for Roho Mtakatifu
0 ratings0 reviews
Book preview
Roho Mtakatifu - Ninah Shali
JEDWALI YA YALIYOMO UKURASA
VICHWA
KUWAPA
SHUKRANI
DIBAJI
UTANGULIZI
SURA YA KWANZA
Roho Mtakatifu ni nani?
Nyakati tatu
SURA YA PILI
Kwa nini Roho Mtakatifu?
SURA YA TATU
Jinsi ya kujazwa na nguvu ya Roho Mtakatifu.
Jinsi ya kutembea na Roho Mtakatifu
SURA YA NNE
Hitimisho.
Vidokezo Vya maombi
KUWAPA
Kitabu hiki kimetolewa kwa Roho Mtakatifu na kwa kila mtu aliye na kiu ya Bwana Yesu Kristo kama mwokozi wake na Roho wa Mungu kama msaidizi. Utukufu na heshima yote kwa Mungu Baba.
Aya za Biblia zimechukuliwa kutoka New King James Version {NKJV} Isipokuwa imeonyeshwa vingine.
Tolea la kwanza Hakimiliki © 2020 na Ninah Shali.
Roho Mtakatifu.
Kitabu hiki hakiwezi kutolewa tena kamili au sehemu kwa njia nyingine yoyote bila idhini ya kuandikwa kutoka kwa mwandishi.Haki zote zimehifadhiwa chini ya sheria ya hakimiliki ya kimataifa.Kwa habari zaidi tafadhali wasiliana na:
Ninah Shali kwa facebook
SHUKRANI
Kwanza kabisa, ningependa kutoa shukrani zangu za dhati kwa mwenyezi Mungu ambaye ameniruhusu kuinjilisha juu ya Roho wake kupitia maandishi haya.
Pili, nawashukuru wazazi wangu wazuri sana, Bwana na Bibi Agripina Majala na familia yangu yote kwa kuwa nami nyakati na misimu yote.Halafu, nawashukuru washauri wangu wote wa kiroho. Sina uwezo wa kuongeza au kupunguza neno ni Mungu tu anayeweza kuwazawadia.Nawashukuru washirika wangu wote katika mwili wa Kristo na kwa watumishi wa Mungu ambao wanainjilisha injili ya kweli ya Yesu Kristo kupitia jumbe zao za maandishi au za sauti ambazo zinanihimiza kiroho kila ninapozisoma au kuzisikiliza.
Shukrani zangu za mwisho ziende kwa kampuni ya uchapishaji na kila atakayesoma kitabu hiki.
Mungi awabariki nyote.
DIBAJI
Tangu utotoni mwangu nilijua (kupitia ndoto, maono, ufunuo) kwamba nina wito wa kumtumikia Mungu lakini sikujua kwa jinsi gani. Wakati fulani maishani mwangu nilijiunga na kusanyiko fulani la kidini {Nyumba ya Watawa} nikitamani kuwa mtawa katika kutafuta wito wangu. Walakini hata huko sikuupata na ikanilazimu kujiondoa. Mnamo Julai, 2009 nilipata maono ambapo nilielekezwa na kuamriwa kuhudhuria ibada ya Kanisa la ukombozi wa mlima Sayuni huko Mombasa Kenya. Siku ya kwanza katika ibada ya kanisa hilo, na kwa muda wote wa ibada siku hiyo, Roho Mtakatifu alinihudumia {machozi yalinitiririka mashavuni mwangu} na kunihukumu kumkubali Yesu Kristo kama Bwana na mwokozi wangu. Papo hapo, amini usiamini, nikakutana na Roho wa Mungu. Sitasahau kamwe jinsi macho na masikio yangu ya kiroho yalivyofunguliwa na kuangazwa kwa mwangaza mkubwa sana ambao uliweka bayana jukumu langu la mbinguni: kuinjilisha injili ya kweli ya Yesu Kristo kwa wanadamu wote ili kuokoa roho kutoka vifungo na kutoka kuzimu. Kuanzia mudo huo, nilianza kuhudhuria mafundisho ya Biblia, kuisoma kwa kina, na kutafakari juu ya neno la Mungu. Nimehudhuria mikutano tofauti ya injili, huduma na ufufuo sio tu kama mshiriki lakini pia kama mtumishi katika mwili wa Kristo. Nimekuwa kwenye mafunzo ya Mungu miaka yote hii. Mwishowe, nimeandika yale ambayo Bwana wangu Yesu Kristo aliniuliza kwa madhumuni ya kushiriki yote ambayo ameweka ndani yangu, kama shoka lake la kiinjili, kueneza injili ya kweli ya Mungu kwa mataifa yote kwa nguvu ya Roho Mtakatifu. Kwa hivyo, unaposoma kitabu hiki, ni ombi langu upate suluhisho za kudumu katika changamoto zako, upate furaha, amani, mwangaza wa kiroho, pia upate maarifa, hekima na ufahamu wa nguvu za Roho Mtakatifu ili kuendeleza ufalme wa Mungu (urithi uzima wa milele), ushawishi na ubadilishe mapenzi yako ili uanze kuishi maisha mazuri. Roho Mtakatifu awe wa kweli kwako kama vile alivyokuwa kwangu katika miaka iliyopita hadi sasa. Naomba utembea katika ushirika wa kina na Roho Mtakatifu, akupe ushindi katika maeneo yote