Mauzauza Ya Raha: Kuchagua Upendo Badala Ya Hofu
By Ken Luball
()
About this ebook
Mauzauza Ya Raha; Kuchagua Upendo badala ya Hofu ni kitabu cha 4 katika ”Tetralojia ya Kuamka”. Kitabu hiki kinafunua njia nyingi za uwongo kupitia maisha ambazo tunaweza kuchukua na jinsi tunaweza kupata amani ya kweli ya ndani na kusudi maishani mwetu.
Wakati uhusiano wetu na ulimwengu unaotuzunguka unapoundwa kupitia lenzi zinazotawala za hofu, Safari yetu ya Maisha mara nyingi inaweza kuwa ya upweke na udhalimu. Shida zetu hazikomi, mizigo yetu ni nzito, mara nyingi hutuongoza kujijengea vizuizi vya ndani, vya kutulinda kutokana na kiwewe cha kihemko. Bado vizuizi vile vile vinatumika kututenga na kila kitu kinachotuzunguka, pamoja na uhalisia wetu.
Mauzauza Ya Raha ni kitabu cha kiroho kinachofunua jinsi ya kukumbatia upendo badala ya hofu, Acha kutafuta maana na furaha ya ndani kupitia shughuli za nje na mahusiano katika ulimwengu; badala yake, kutafuta kutoka ndani.
Related to Mauzauza Ya Raha
Related ebooks
Mwongozi Wa Roho: Safari Maishani Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsLeo Nitakufa: Chaguo Maishani Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNjia za Utu kuelekea kwa Furaha: Hekima vitendo (Swahili Version) Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsNdoa ya Mfano Wa Kuigwa Rating: 4 out of 5 stars4/5Ufufuo & Uchukuo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsSayansi ya Kupata utajiri Rating: 5 out of 5 stars5/5Mafundisho ya Ndoa Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsStadi Ya Uongozi Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHistoria & Maisha ya Yeshua Kristo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsHawara Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsYisrael Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsJinsi ya Kusali & Kuongea na Yahweh Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMafundisho ya Utajiri Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsSiri ya Kifo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMwana-Adam ni Nani Naye ni Nini Mungu Amkomboe: Chuo cha Kwanza, #1 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsVile Unavyopaswa Kuwa: kujitambua na kuchukua hatua: Kujitambua, #1 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsUjio wa Pili wa Yesu Kristo Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsRoho Mtakatifu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWale Wana ambao ni Hatari Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsUtatu Mtakatifu Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsWengine... Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsKatika Eneo la Adui Kuokolewa na Silaha ya Siri: Swahili Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsDini ya Fedha Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsUanzishaji Wa Imani: Taasisi ya mafunzo ya Isaya 58 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsImani Ya Mtu Wingine Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMSHINDI WA KILA LEO: MHOFIE MWANAO ASISHINDWE.: ELIMU NJE YA DARASA, #1 Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsJivutie Upako Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMguso Mzuri Wa Upako Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMisingi ya Imani Rating: 0 out of 5 stars0 ratingsMbinu za Kupata Mume Mwema Rating: 0 out of 5 stars0 ratings
Reviews for Mauzauza Ya Raha
0 ratings0 reviews
Book preview
Mauzauza Ya Raha - Ken Luball
Mauzauza Ya Raha :
––––––––
KUCHAGUA UPENDO BADALA HOFU
––––––––
Riwaya ya Kiroho na Ken Luball
& Bodhi ( Mwongozo wa Kiroho
)
Translator: Samwel Lubisia
Copyright Claimant: Ken Luball
Ujumbe wa mwandishi:
Nini Maana ya Uzima?
Maana ya uzima,
Sababu tupo hai,
Ni kuisikiliza kwa makini Roho aliye ndani yetu ,
Na kuifuata katika njia atakayotuongoza.
Vipo vitabu vinne katika Tetralojia ya Kuamka
:
Leo Naenda Kufa: Uchaguzi Maishani
Mwongozo wa Roho: Safari Maishani
Utulivu: Kijiji Cha Matumaini
Mauzauza ya Raha: Kuchagua Upendo badala ya Hofu
Maisha ya kiroho hali ya ni kuamini yuko Mungu (Roho au Nafsi) katika kila maisha, na kwa sababu hii maisha ya kila mmoja ni muhimu , ni sawa na yameunganishwa.
Lengo langu la kukiandika kitabu hiki ni Kuwaamsha na kuwasaidia wengine, Walioamka, huelewa kikamilifu maana ya Kuiona Nuru, na kwa hivyo, Safari yao katika Maisha yaweza kutambulika kikamilifu.
Hadithi tatu zimeandikwa katika nafsi ya kwanza, kufuatilia safari ya Kiroho
Maishani mwa mtoto. Wanapopata mafunzo ya jinsi ya kuyajibu maswali hayo [niliyouliza mwanzo] kwa njia ya kueleweka, kuvutia, na ya kipekee, ambayo sio tu ya kufikirisha bali pia kusisimua.
Bodhi ni Mwongozo wangu wa Kiroho
; ananizungumzia kwa urahisi huku nikiandika mawazo yake. Japo safari yangu ya Kuiona Nuru, haijakamilika, Bodhi, akiwa Mwongozo wa Roho, Bila Shaka Amelimika. Tulikiandika kitabu hiki kwa ajili ya wote wanaotaka kuianza safari ya Kuamka au Wameamka na wanatafuta njia ya Kuiona Nuru
Ni kwa upendo tu na msaada wa Bodhi
tuliweza kuviandika vitabu hivi kwa pamoja
Ili kufahamu mengi kuhusu vitabu vyote vinne vya Kiroho katika tovuti yangu http://kenluball.com
Yaliyomo
Dibaji: Kwa watoto wa ulimwengu
Chapter 1: Kutafuta Mwanga Wako
Chapter 2: Utangulizi wa Uhusiano Akili, Mwili na Roho
Chapter 3: Ukuta, Barakoa na Mlango
Chapter 4: Uhusiano wa Akili, Mwili na Roho
Chapter 5: Roho Anayapa maisha yetu Maana
Chapter 6: Roho na Kiona Nuru
Chapter 7: Kuishi katika Nuru
Chapter 8: Kuchagua Upendo badala ya Hofu
Chapter 9: Kuishi na Roho
Chapter 1: Mauzauza ya Raha
Chapter 11: Maana ya maisha
Hitimisho
Nyongeza Tafakari za Kiroho
Kuruhusu Ken
Kwa ajili ya Watoto wa Dunia
Tunakitoa kitabu hiki kwa ajili ya Watoto wa Dunia. Ni matumaini yetu kwamba wazazi wako, na wote unaowapenda, watakisoma kitabu hiki na kwa kufanya hivyo, wataweza kukusaidia Kuchagua njia yako maishani kwa busara. Ni matumaini yetu kwamba safari yako itajazwa na upendo, furaha na ya kukushangaza.
Dibaji:
Kwa Ajili ya Watoto wa ulimwengu
Unavyoendelea kuwa mkubwa,
Utagundua maisha yana changamoto
Ulimwengu sio mahali pazuri sana kuishi siku zote
Utaona mambo mengi na kushangaa
Ni kwa nini mabaya huwafanyikia wengi
Utawaona wasio na chakula cha kutosha
Au mahali pa kuishi, na wengine
Wasiopenda mtu kwa sababu yuko tofauti.
Tofauti na picha ya hapo juu, bila kujali rangi yako ya ngozi ni gani,
Nchi unayoishi, jina lako, dini,
Au tofauti zozote zilizopo,
Ni muhimu kutoamini yeyote ni bora zaidi
Au wa maana zaidi kumliko mwingine.
Kila maisha ni ya maana [kwa kiwango sawa]
Bila ya kujali tofauti zozote zilizopo kati yetu
Kuishi maisha Mazuri haihusiani lolote na kazi uliyonayo,
Wala pesa unazopata,
Kuwa mashuhuri au lingine lolote unaloweza kusikia
Unapokua mkubwa.
Ila la muhimu ni kwamba wewe ni mtu mzuri
.
Kuwa mtu anayejali hisia za wengine
Kuwasaidia unapoweza,
Kuwatendea wote kwa wema na upendo,
Hata kama wao hawakutendei hivyo.
Utawapata wengi ulimwenguni wasio na furaha,
Wanajijali wenyewe tu.
Tafadhali usiwe
kama wao
Unaweza kuubadili ulimwengu kama tu utaisikiliza
Sauti nyamavu moyoni mwako na
Kushiriki ujumbe huo na wote.
Kumbatia maishani kwa heshima na unyenyekevu.
Kua mkarimu kwa kila mtu
Shirikisha uzuri ulio moyoni mwako na wote waliotofauti au
Wanapambana
Na muhimu zaidi, watendee wengine
Jinsi ungependa utendewe
Ukifanya hivi, utakua mwenye furaha.
Usichague kuishi ulimwengu ambao kila mtu ana hofu,
Kujihofia wenyewe tu.
Ila wajali wengine, kuwa mkarimu, mwenye huruma, upendo, heshima, mnyenyekevu, mwenye subira, mwema, mwenye shukurani na matumaini maishani.
Kuwa mjasiri; jali hisia za wengine,
Kuwa mtu mwenye urafiki na uwasaidie wakiwa tofauti au wakiwa wahitaji
Ukifanya hivi, unaweza kutapata maisha yako yakawa yenye furaha na maana.
Njia unayoichagua maishani itaamua
Mustakabali wa Dunia.
Kizazi cha zamani hakijafanya kazi nzuri sana
Kuilinda sayari yetu na [kuwalinda] wenzao
Ni juu yako, kufanya mabadiliko
Ambayo lazima yafanywe
Kwa kuchagua njia iliyo sawa maishani .
"Maono yako yatakuwa wazi tu
Utakapotazama ndani ya moyo wako
Atazamaye nje, huota ndoto.
Atazamaye ndani, huamka"
Carl Jung
Sura Ya 1:
Kupata Mwanga Wako
Majibu tunayoyatafuta, ili kupata mwanga wako
,
Unaotuwezesha kukumbatia amani ya ndani,
Upendo na maana maishani mwetu,
Huenda yasiwahi patikana kwa kutazama nje.
Ila kwa kujitazama ndani alipo Roho,
Kukubali na Kuruhusu Roho kuongoza safari
Yako maishani, hata hivyo zipo changamoto.
Hii ni kwa sababu ya kutawaliwa na hali ya [1]Ego.
Ego ambayo tumefunzwa
na kuamini
tangia kuzaliwa kwetu.
Kuamka
huanza pindi tunapoanza kudadisi kuhusu kila ambacho tulijifunza
.
Nuru
huja baada ya kukubali
ukweli kwamba
Yote tuliyojifunza hayakuwa sawa
.
Safari hii ni ndefu, ngumu na mara nyingi yenye upweke.
Maana ya uzima
ni kufunga safari hii,
kujitolea kushiriki bila ubinafsi
Kushiriki pamoja na wengine mwanga
ulio ndani yetu.
"Ni kwa nini tuko hai? Je
Nini maana ya kua hai na uzima"? Maswali haya yameulizwa kwa miaka elfu moja, yaweza kushangaza jinsi majibu yake ni rahisi. Tunapozaliwa, majibu yake tayari yalikuwa ndani yetu. Kwa hakika, pindi tu tunapozaliwa majibu ya hayo maswali yanatokomea katika changamoto ambazo sote hupitia maishani.
"Miaka mitano ya kwanza katika Maisha ya kila mtoto ni ya maana sana". Katika muda huu
[mtoto] hujifunza ambayo yanatarajiwa kutoka kwao na jinsi atakavyo chukulia hali tofauti ulimwenguni.
Wakati huu pia wanaendeleza mtazamo wa kijumla jinsi vile watawachukulia wenzao. Maoni yao, dhana, Imani, Pamoja na matarajio hujengwa wakati huu na kujenga msingi jinsi watakavyo watendea na kuwachukulia wengine maishani mwao.
Katika miaka hii, ikiwa mtoto atafunzwa kuutazama ulimwengu na watu wengine kwa njia mche wa giza na uhasi, pale ambapo "Hofu hutawala
Upendo ", basi watakumbana na changamoto si haba. Kwa kuutazama ulimwengu kwa jinsi hii, wanajifunza ubinafsi na kutowajali wengine. Safari yao maishani huwa yenye upweke na masumbuko pamoja na mapambano.
Kwa upande mwingine hata hivyo, ikiwa watakumbatia na kutawaliwa na "Upendo Wala si Hofu , basi Maisha yao huchukua mwelekeo tofauti. Kwa kukumbatia msingi wa upendo na maana yake, wanaanza kuyaelewa Maisha katika njia tofauti, njia isiyo ya ubinafsi bali ya kuwaonea huruma
watu wote". Watoto hawa huwaelewa na kuwaheshimu wengine na pia kujenga mtazamo wa Maisha wa upendo bali sio wa hofu na chuki.
"Anayojifunza mtoto katika miaka yake mitano ya kwanza, yaweza kuadhiri Maisha yake yote"
Masumbuko mengi tulio nayo maishani huja kama athari za Imani tulizo jenga katika miaka hii ya utotoni. Miaka tunayo shawishika kirahisi tukiwa Watoto. Tunajifunza kuhusu mahusiano yetu na ulimwengu kisha tunaanza kujaribu kuyaondoa madhara haya Maisha yetu yote. Madhara haya husababishwa na kuzikubali jumbe za uongo na ubinafsi kama jumbe za kweli na halisi, tunapoendelea kukubali majukumu yetu ulimwenguni. Anapofika umri wa kuanza shule [mtoto], mara nyingi jumbe hizi huwa zimehifadhiwa ndani yake na huchangia katika kushawishi mawazo na matendo yake [mtoto] katika Salio la Maisha yake.
Ningependa tuangazie mfano wa mkoba ulio funguka. Kabla hatujazaliwa mkoba huu hauna chochote. Pindi tu tunapozaliwa, Ego na kila tunayoamini kuwa kweli, yanaanza kuujaza mkoba huu. Katika kutangamana kwetu, mkoba unaendelea kua mzito tunavyo endelea kuujaza na mizigo yetu kutokana na tunayojifunza maishani mwetu. Kadri mkoba huu unavyoendelea kua mzito, ndivyo pia Mwanga wetu unazidi Kufifia, na hivyo kuna haja ya kupunguza na kuondoa mizigo tunapoanza Kuamka na kuianza safari yetu kuelekea kwenye Nuru.
Katika mkoba huu umejaa ubinafsi usio wa kweli tuliojifunza kua kweli wakati tulipokua watoto. Ingawa mkoba huu wahitaji mda kidogo tu kujazwa, yaweza kuchukua maisha yao yote "kutafuta mwanga wao" tena, kuiondoa mizigo na kuirejelea hali ya awali ya utulivu wa ndani, na ufahamu ambao mwanzoni waliujua kabla mkoba haujaanza kujaa; kabla Nafsi ya mtoto kujifunza mengi yasiyo kweli na kukubalika kama kweli. Kadri wanavyoubeba mkoba mzito, ndivyo pia safari yao maishani inakuwa ngumu na pia inakua vigumu zaidi kutafuta mwanga wao mara tena.
Mikoba yetu mingi hujazwa utotoni katika miaka ya kwanza mitano. Kisha tunajaribu maishani mwetu kuiondoa mizigo hii.
Tunapotafuta mwanga
wetu na kuanza kudadisi ukweli wa yote tuliyofunzwa katika miaka hii, Basi tunaanza Kuamka na kuanza kazi ngumu ya kuondoa mizigo katika mikoba yetu.